Saturday, October 22, 2016

KAMATI KUU CHADEMA KUFANYA KIKAO CHA SIKU MBILI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ​




Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa Kamati Kuu ya Chama itakutana kwa siku mbili, kuanzia Oktoba 22-23, mwaka huu, katika kikao chake cha kawaida.

Kikao hicho kitakachofanyika jijini Dar es Salaam, pamoja na agenda mbalimbali, kitapokea na kujadili kwa kina taarifa ya hali ya siasa nchini na mwelekeo wa nchi kwa ujumla kiuchumi na kijamii.

Aidha, Kamati Kuu pia itapokea na kujadili taarifa ya fedha na Mpango wa Uchaguzi wa Kanda 10 za Chama, kabla ya Sekretarieti kuanza utekelezaji, ambao utahusisha kuwa na shughuli za chama, kisiasa na kiutendaji, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwatumikia wananchi, operesheni za uimarishaji wa chama nchi nzima na kuendelea kutoa elimu ya uraia.

Imetolewa leo Ijumaa, Oktoba 21, 2016 na;

Tumaini Makene Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano CHADEMA

No comments:

Post a Comment