Sunday, May 26, 2013
Saturday, May 25, 2013
Suala la Mtwara ni zaidi ya Gesi asilia - Kutumia nguvu ya dola sio njia pekee ya Amani - Zitto Kabwe
Serikali iangalie upya namna inavyolitazama suala la Mtwara. Hivi sasa suala hili linaonekana kiusalama zaidi badala ya kuliona kama suala la kijamii na maendeleo lenye kuhitaji kujenga imani ya wananchi.
Suala hili linahitaji muda na heshima kwa wananchi. Ni vema tuache sauti ya wananchi kusikika na kuzitolea maamuzi sahihi yenye kujenga kuaminiana na kuheshimiana kati ya dola na wananchi.
Suala la Mtwara ni zaidi ya gesi asilia. Ni matokeo ya kutengwa kimaendeleo kwa muda mrefu. Suala la Gesi ni nafasi ya kuunganisha watu wa kusini na Jamhuri ya Muungano. Tuamue sasa kufanya maamuzi sahihi na kuunganisha Jamhuri yetu au kukosea na kudharau na kuivunja Jamhuri yetu.
Kama Kuna mataifa ya kigeni/makampuni binafsi yanahusika na hali ya Mtwara. Serikali iyataje mataifa hayo na makampuni hayo hadharani na vibaraka wao.Vinginevyo nadharia hizi zitaonekana ni ni propaganda tu kwa lengo la kufunika kombe mwanaharamu apite.
Nadharia zote za kuelezea masuala ya Mtwara zinakimbia suala la msingi ie kutengwa kwa muda mrefu sana kwa mikoa ya kusini kwenye maendeleo ya nchi. Ahadi za Rais Ben Mkapa kuhusu Mtwara Corridor, ahadi za Rais Jakaya Kikwete za 2005 na biashara ya korosho ni miongoni mwa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa Mtwara. Suala hili la msingi lazima lipatiwe majawabu mwafaka kwa maelezo yenye heshima kwa wananchi badala ya dharau na vijembe dhidi ya raia.
Kuna kukosa imani kukubwa kwa wananchi dhidi ya Serikali. Suala hili ni pana zaidi na linasambaa Tanzania nzima. Malalamiko yanaposhawishiwa kihofu tu huleta matatizo makubwa sana. Hali ya namna hii haijawahi kutokea nchini mwetu. Kukamata na kufunga viongozi wa wananchi haitosaidia kamwe.
Kutumia nguvu ya dola kuzima vuguvugu la wananchi sio njia pekee ya kujenga amani. Makovu ya kutumia nguvu ya dola huchukua muda mrefu sana kupona. Lazima kubadili mkakati wa kuongoza na kuliweka Taifa sawa.
Zitto Zuberi Kabwe (Mb)
24th May 2013
Suala hili linahitaji muda na heshima kwa wananchi. Ni vema tuache sauti ya wananchi kusikika na kuzitolea maamuzi sahihi yenye kujenga kuaminiana na kuheshimiana kati ya dola na wananchi.
Suala la Mtwara ni zaidi ya gesi asilia. Ni matokeo ya kutengwa kimaendeleo kwa muda mrefu. Suala la Gesi ni nafasi ya kuunganisha watu wa kusini na Jamhuri ya Muungano. Tuamue sasa kufanya maamuzi sahihi na kuunganisha Jamhuri yetu au kukosea na kudharau na kuivunja Jamhuri yetu.
Kama Kuna mataifa ya kigeni/makampuni binafsi yanahusika na hali ya Mtwara. Serikali iyataje mataifa hayo na makampuni hayo hadharani na vibaraka wao.Vinginevyo nadharia hizi zitaonekana ni ni propaganda tu kwa lengo la kufunika kombe mwanaharamu apite.
Nadharia zote za kuelezea masuala ya Mtwara zinakimbia suala la msingi ie kutengwa kwa muda mrefu sana kwa mikoa ya kusini kwenye maendeleo ya nchi. Ahadi za Rais Ben Mkapa kuhusu Mtwara Corridor, ahadi za Rais Jakaya Kikwete za 2005 na biashara ya korosho ni miongoni mwa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa Mtwara. Suala hili la msingi lazima lipatiwe majawabu mwafaka kwa maelezo yenye heshima kwa wananchi badala ya dharau na vijembe dhidi ya raia.
Kuna kukosa imani kukubwa kwa wananchi dhidi ya Serikali. Suala hili ni pana zaidi na linasambaa Tanzania nzima. Malalamiko yanaposhawishiwa kihofu tu huleta matatizo makubwa sana. Hali ya namna hii haijawahi kutokea nchini mwetu. Kukamata na kufunga viongozi wa wananchi haitosaidia kamwe.
Kutumia nguvu ya dola kuzima vuguvugu la wananchi sio njia pekee ya kujenga amani. Makovu ya kutumia nguvu ya dola huchukua muda mrefu sana kupona. Lazima kubadili mkakati wa kuongoza na kuliweka Taifa sawa.
Zitto Zuberi Kabwe (Mb)
24th May 2013
CHADEMA yamng’ang’ania Kinana
NI MELI ZAKE KUHUSISHWA BIASHARA YA PEMBE ZA NDOVU
KAMBI Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA, kwa mara nyingine imezidi kumbana Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ikimtaka mwendesha mashitaka wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kumfungulia mashitaka ya kutorosha pembe za ndovu katika mahakama ya Afrika Mashariki.
Akiwasilisha maoni ya kambi hiyo jana kwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2013/2014, Raya Ibrahim Khamis kwa niaba ya msemaji mkuu Ezekiel Wenje, alitaka Tanzania iombe msaada wa Kenya yenye ubalozi wa Vietnam ili kurahisisha upatikanaji wa ushahidi badala ya kutegemea ubalozi wake ulioko China.
Raya alisema madhumuni ya kumfungulia kesi Kinana yana lengo la kuudhibiti mtandao wa majangili na wafanyabiashara haramu ya pembe za ndovu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Alibainisha kuwa wanataka Kinana afunguliwe kesi kutokana na meli anazosimamia mojawapo ilikamatwa na shehena za pembe za ndovu huko Vietnam mwaka 2009.
Hii ni mara ya pili kwa kambi hiyo kuibua tuhuma hizo dhidi ya Kinana ambapo kwa mara ya kwanza msemaji mkuu wa kambi ya upinzani kwa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa alihoji jambo hilo na kupata upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa CCM.
Raya alisema kuwa biashara haramu ya pembe za ndovu katika ukanda wa Afrika Mashariki inakua kwa kasi jambo linalotishia kutoweka kwa wanyama ndovu ambao ni kivutio kikubwa cha utalii.
Bonyeza Read More Kuendelea
Friday, May 24, 2013
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE . EZEKIAH DIBOGO WENJE (MB) KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2012/2013 NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA AFRIKA MASHARIKI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014
1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeundwa na Ibara ya 2(1) ya Mkataba
wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kufuatia makubaliano ya wakuu wa nchi
wanachama wa jumuiya hiyo ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Aidha Ibara ya 8(3) (a) ya Mkataba wa kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki imezipa mamlaka
nchi wanachama kuanzisha Wizara mahsusi, itakayoshughulikia masuala ya Afrika
Mashariki. Kwa mujibu wa ibara hiyo, Tanzania, ilianzisha Wizara ya Afrika Mashariki ambayo majukumu yake ni pamoja utekelezaji wa Mkataba
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mikataba Midogo (Protocols) Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja la Afrika
Mashariki na Mazungumzo ya uundwaji wa
Shirikisho la kisiasa la Afrika
Mashariki.
Mheshimiwa Spika, ni mategemeo ya Watanzania kwamba, Wizara hii ya Afrika Mashariki
italitendea haki taifa hili, kwa kuwashirikisha wananchi kwenye kila hatua na kwa
kusimamia kwa dhati na kikamilifu michakato yote ya mtangamano wa Afrika
Mashariki, kwa maslahi ya nchi yetu, ili kuhakikisha kwamba Tanzania inanufaika
vilivyo na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani kipindi hiki itajielekeza kwenye mambo
machache ambayo tunaamini yakizingatiwa, Jumuiya ya Afrika Mashariki itakuwa
imara, na nchi zote wanachama watafurahia matunda ya jumuiya hiyo.
2.0 MADAI YA MAFAO
YA WASTAAFU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI ILIYOVUNJIKA 1977
Mheshimiwa Spika, madai ya mafao ya wazee wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika
Mashariki sasa ni aibu kwa Taifa. Wastaafu hawa wameyumbishwa kiasi cha
kutosha, wamepuuzwa kiasi cha kutosha, wamedhalilishwa kiasi cha kutosha na
wameonewa kiasi cha kutosha na serikali hii ya CCM inayojiita sikivu. Hakika
laana ya wastaafu hawa wanaodhulumiwa haki yao wazi wazi namna hii itaendelea kulitafuna taifa hili kwa kwa miaka
mingi ijayo kama Serikali haitawatendea haki.
Mheshimiwa Spika, Baada ya Jumuiya hiyo kuvunjika ghafla tarehe 30 Juni, 1977
ulizuka mgogoro wa mgawanyo wa mali na madeni yake. Ili kuumaliza mgogoro huo,
Umoja wa Mataifa uliiteua Benki ya Dunia kusuluhisha mgogoro huo. Benki ya
dunia ilimteua mtaalamu wake, mwanadiplomasia, Dkt. Umbricht (sasa marehemu) ambaye alifanikisha kuwanzishwa kwa
Mkataba wa Kimataifa uliojulikana kama “East African Community Mediation Agreement
1984” kuhusu mgawanyo wa mali na madeni ya Jumuiya yakiwemo mafao ya
wafanyakazi wa Jumuiya hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa tulizo nazo, kazi kubwa aliyofanya
msuluhishi, Dkt. Umbritch ilikuwa ni kuzigawanya fedha za pensheni na provident
funds za Jumuiya kwa nchi tatu wanachama yaani Kenya, Uganda na Tanzania
kulingana na idadi ya raia wake katika Jumuiya, kwa madhumuni ya kuwalipa mafao
raia wake. Katika mgawo huo, Tanzania ilikabidhiwa paundi za Uingereza milioni
14 kwa ajili ya kulipa mafao ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika
Mashariki. Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kulieleza bunge hili na
wananchi wote fedha hizo zilitumika kufanyia nini kama walengwa hawakulipwa
mafao yao?
Mheshimiwa Spika, nchi za Kenya na Uganda tayari zilishawalipa wastaafu wa Afrika
ya Mashariki stahili zao na hali huko ni shwari, lakini kwa Tanzania jambo hili
limegubikwa na wingu zito la ufisadi kwa kuwa fedha ya kuwalipa wastaafu hao
ilishatolewa. Kwanini wastaafu hao hawakulipwa, na wale waliolipwa, walipewa
cheki za silingi 10 na shilingi 130 za kitanzania jambo ambalo ni aibu na
fedheha kwa Serikali hii ya CCM inayojiita sikivu kwa wananchi wake.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali hii ya CCM inayojiita
sikivu, kutoa tamko leo, mbele ya bunge
hili kuhusu mafao ya wastaafu hao ili wajue moja: kama wanalipwa au hawalipwi. Kama Serikali haitatoa tamko leo, kuhusu unyanyasaji wanaofanyiwa wastaafu wa
Afrika Mashariki, basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni italazimika kuleta hoja
binafsi bungeni kwa hatua za kibunge kuhusu mafao ya wastaafu wa iliyokuwa
Afrika Mashariki.
Bonyeza Read More Kuendelea
Rufaa ya Mahimbo dhidi ya mchumba wa Dk. Slaa yatupwa
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Aniseth Wambura, akieleza kwamba mahakama yake imefikia uamuzi wa kuitupilia mbali rufaa hiyo kwa sababu haina mantiki ya kisheria.
Alisema mahakama imekubaliana na hukumu iliyotolewa Aprili mwaka jana na Mahakama ya Mwanzo Sinza katika kesi ya madai ya talaka iliyokuwa imefunguliwa na Mushumbusi.
Mahakama hiyo ya chini ilitangaza kuwa hakukuwa na ndoa baina ya watu hao kwasababu Mahimbo alikuwa ni mzinzi, simwaminifu katika ndoa yake na alikuwa akimtesa mkewe.
Hakimu Wambura alisema baada ya mahakama yake kusikiliza hoja za mwomba rufaa na mjibu rufaa, mahakama imefikia uamuzi wa kukubali hoja za Mushumbisi kuwa kwa tabia mbaya ya uzinzi na ukosefu wa uaminifu katika ndoa yake hapakuwapo na ndoa baina yao hivyo inatangaza kuwa hukumu ya Mahakama ya Mwanzo Sinza ambayo iliivunja ndoa hiyo ilikuwa hukumu sahihi.
Baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, wakili anayemtetea Mshumbuzi, Philemon Mutakyamilwa alisema amefurahishwa na hukumu hiyo kwani mahakama imetenda haki kwasababu kesi hiyo ya madai ya talaka ilikuwa na msukumo wa siasa chafu zilizokuwa na lengo la kumchafulia jina mteja wake (Mshumbusi) ambaye kwa sasa ni mzazi mwenza wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa.
Wamemdharau Nyerere na Kuivunja Misingi - Sasa hawana pa Kushikilia!
Kwao Nyerere siyo "Baba wa Taifa" tena; kwao ni "Mzee Nyerere"; kwa watawala wetu hawa walioshindwa wanasema wamefanya mambo mengi sana ya maendeleo kkuliko "Wakati wa Nyerere". Wanajitamba kuwa wao wamekuza sana demokrasia na kuwa hata "Nyerere" hakuweza kufanya waliofanya wao. Katika upotofu wao wanaamini kabisa kuwa wao wanapendwa zaidi; na wanapendwa kwa sababu wamefanya mengi mno na hawaelewi kwanini watu hawaoneshi shukrani!
Ndio maana kila kukicha hawaachi kubembeleza kwa wananchi kuwa "hamuoni tunayofanya" na kuwa watu wanalaumu tu lakini hawatoi pongezi kwa "mazuri mengi". Imefika mahali Kikwete mwenyewe amedai mahali fulani anataka kukumbukwa kuwa ni "bwana maendeleo"; anasema hivi kwa sababu anapokaa ofisini anaamini kabisa kuwa ameweza kuwapatia Watanzania 'vitu" vingi sana vya maendeleo kuliko wakati wowote wa historia - vitu ambavyo hata Nyerere hakuweza kuwapatia. Kikwete anataka awe juu ya Nyerere kwa kila kipimo kwani kipimo kilichowekwa ni Nyerere. Na bila ya shaka kuna sababu - Nyerere hakuamini kuwa walikuwa tayari kuwaongoza Watanzania - hawa kina Kikwete na Lowassa.
Sasa katika kumdunisha Nyerere ili wao wakue wameacha propaganda chafu dhidi ya Nyerere na uongozi wake. Leo hii tunashuhudia mambo ambayo - pamoja na 'ubaya' wote wa Nyerere hayakuwahi kutokea chini ya "dhaalim Nyerere"! Matukio yanayotokea leo hii ukiwaambia watu walioshi wakati wa Nyerere, chini ya chama kimoja na uongozi thabiti hawawezi kuelewa yanawezekana vipi kutokea. Watu wa enzi za Mwalimu wanakumbuka vizuri kuwa kiongozi aliyefanya madudu hakuvumuliwa; na bahati mbaya wakati ule hatukuwa na wasomi wengi na watu wengi wenye udhoefu lakini Nyerere hakuwaonea huruma. Wapo ambao hadi leo wana kinyongo na Nyerere kwa sababu hakuwapa nafasi nyingine.
Lakini katika kumdharaulisha Nyerere na kujaribu kupuuza mafanikio yake makubwa zaidi wamejikuta hawana pa kukimbilia! Tuliokuwa wakati wa Nyerere hatukumbuki jinsi JWTZ likitumiwa kisiasa kama linavyotumika hivi sasa! Fikiria ndege ya jeshi itumwe kumchukua raia kumpeleka Mahakamani!? Kwamba, ati vurugu za uchaguzi zilazimishe JWTZ kuingilia kati! Kwamba vikosi vya kutuliza ghasia vya polisi vizidiwe nguvu na mara moja kuliingiza jeshi kufanya kazi za jeshi la polisi! Unthinkable! Lakini wao wanaamini wako sawa!
Lakini siyo kwamba wamedharaulisha na kumtupa nje Nyerere ni zaidi ya hivyo; wameitupa misingi ya taifa letu. Wanataka kujenga kwa misingi ya mabua! Waliachiwa misingi ya zege lakini wao wakiamini ni 'magenius" wameamua kutengeneza 'taifa jipya' nje ya misingi iliyounda Tanzania. Leo hii Watanzania kwa mamilioni wananung'unika moyoni kwani hawatambui kama hili ndilo Taifa waliloachiwa kama urithi. Sasa hivi inaonekana Tanzania inazidi kufanana zaidi na mataifa mengine ya Afrika kiasi kwamba linaweza lisitofautike tena mbele ya umma.
Wameitupa misingi sasa hawana cha kujengea; wamebakia kutumainia vitisho, dharau na matumizi ya nguvu. Wameshindwa kabisa kujenga hoja - kwa mfano kwenye hili suala la gesi. Hawana ushawishi wa hoja na badala yake hata kauli zao wanazotoa zimejaa dharau (contempt) na matokeo yake watu nao wanawadharau! Wanafikiri vitisho na kejeli zinajibu hoja!
Kushindwa kwa sera zao mbalimbali ni matokeo ya kuachana na misingi ya taifa; wanafikiri wanaweza kutengeneza sera nzuri nje ya misingi ya taifa! Matokeo yake:
Sera ya Nishati na Madini imeshindwa
Sera yao ya Gesi imeshindwa - hata kabla haijaanza!
Sera yao ya Elimu imeshindwa
Sera yao ya siasa imeshindwa
Sera yao ya Sayansi na Teknolojia imeshindwa
Sera yao Mazingira imeshindwa
N.k
Wameshindwa lakini hawaamini wameshindwa na badala yake wanawalaumu wanaowaambia wameshindwa kwa kushindwa kwao! Kana kwamba, wanaowalaumu wakinyamaza basi wao wataweza! Wenyewe wanaambizana kuwa wakipewa nafasi nyingine 2015 basi wataaanza kuweza; na wapo watu wanaamini kuwa hilo linawezekana; kwamba pundamilia anaweza kugeuka na kuwa farasi! Kama wenyewe wameshindwa kuvuana magembe licha ya mbwembwe zote za "kuvuana magamba" kweli kuna uwezekanow wataweza? Na ukweli ni kuwa walipofika sasa hawawezi kurudi kwenye misingi ya Nyerere na Taifa letu; kwa sababu kurudia misingi hiyo ni kujishtaki katika historia.
kuna namna moja ttu ya kuwasaidia... kuendelea kuwakataa.
Maskini CCM!
Maskini Kikwete
Maskini Tanzania chini yao!
Ndio maana kila kukicha hawaachi kubembeleza kwa wananchi kuwa "hamuoni tunayofanya" na kuwa watu wanalaumu tu lakini hawatoi pongezi kwa "mazuri mengi". Imefika mahali Kikwete mwenyewe amedai mahali fulani anataka kukumbukwa kuwa ni "bwana maendeleo"; anasema hivi kwa sababu anapokaa ofisini anaamini kabisa kuwa ameweza kuwapatia Watanzania 'vitu" vingi sana vya maendeleo kuliko wakati wowote wa historia - vitu ambavyo hata Nyerere hakuweza kuwapatia. Kikwete anataka awe juu ya Nyerere kwa kila kipimo kwani kipimo kilichowekwa ni Nyerere. Na bila ya shaka kuna sababu - Nyerere hakuamini kuwa walikuwa tayari kuwaongoza Watanzania - hawa kina Kikwete na Lowassa.
Sasa katika kumdunisha Nyerere ili wao wakue wameacha propaganda chafu dhidi ya Nyerere na uongozi wake. Leo hii tunashuhudia mambo ambayo - pamoja na 'ubaya' wote wa Nyerere hayakuwahi kutokea chini ya "dhaalim Nyerere"! Matukio yanayotokea leo hii ukiwaambia watu walioshi wakati wa Nyerere, chini ya chama kimoja na uongozi thabiti hawawezi kuelewa yanawezekana vipi kutokea. Watu wa enzi za Mwalimu wanakumbuka vizuri kuwa kiongozi aliyefanya madudu hakuvumuliwa; na bahati mbaya wakati ule hatukuwa na wasomi wengi na watu wengi wenye udhoefu lakini Nyerere hakuwaonea huruma. Wapo ambao hadi leo wana kinyongo na Nyerere kwa sababu hakuwapa nafasi nyingine.
Lakini katika kumdharaulisha Nyerere na kujaribu kupuuza mafanikio yake makubwa zaidi wamejikuta hawana pa kukimbilia! Tuliokuwa wakati wa Nyerere hatukumbuki jinsi JWTZ likitumiwa kisiasa kama linavyotumika hivi sasa! Fikiria ndege ya jeshi itumwe kumchukua raia kumpeleka Mahakamani!? Kwamba, ati vurugu za uchaguzi zilazimishe JWTZ kuingilia kati! Kwamba vikosi vya kutuliza ghasia vya polisi vizidiwe nguvu na mara moja kuliingiza jeshi kufanya kazi za jeshi la polisi! Unthinkable! Lakini wao wanaamini wako sawa!
Lakini siyo kwamba wamedharaulisha na kumtupa nje Nyerere ni zaidi ya hivyo; wameitupa misingi ya taifa letu. Wanataka kujenga kwa misingi ya mabua! Waliachiwa misingi ya zege lakini wao wakiamini ni 'magenius" wameamua kutengeneza 'taifa jipya' nje ya misingi iliyounda Tanzania. Leo hii Watanzania kwa mamilioni wananung'unika moyoni kwani hawatambui kama hili ndilo Taifa waliloachiwa kama urithi. Sasa hivi inaonekana Tanzania inazidi kufanana zaidi na mataifa mengine ya Afrika kiasi kwamba linaweza lisitofautike tena mbele ya umma.
Wameitupa misingi sasa hawana cha kujengea; wamebakia kutumainia vitisho, dharau na matumizi ya nguvu. Wameshindwa kabisa kujenga hoja - kwa mfano kwenye hili suala la gesi. Hawana ushawishi wa hoja na badala yake hata kauli zao wanazotoa zimejaa dharau (contempt) na matokeo yake watu nao wanawadharau! Wanafikiri vitisho na kejeli zinajibu hoja!
Kushindwa kwa sera zao mbalimbali ni matokeo ya kuachana na misingi ya taifa; wanafikiri wanaweza kutengeneza sera nzuri nje ya misingi ya taifa! Matokeo yake:
Sera ya Nishati na Madini imeshindwa
Sera yao ya Gesi imeshindwa - hata kabla haijaanza!
Sera yao ya Elimu imeshindwa
Sera yao ya siasa imeshindwa
Sera yao ya Sayansi na Teknolojia imeshindwa
Sera yao Mazingira imeshindwa
N.k
Wameshindwa lakini hawaamini wameshindwa na badala yake wanawalaumu wanaowaambia wameshindwa kwa kushindwa kwao! Kana kwamba, wanaowalaumu wakinyamaza basi wao wataweza! Wenyewe wanaambizana kuwa wakipewa nafasi nyingine 2015 basi wataaanza kuweza; na wapo watu wanaamini kuwa hilo linawezekana; kwamba pundamilia anaweza kugeuka na kuwa farasi! Kama wenyewe wameshindwa kuvuana magembe licha ya mbwembwe zote za "kuvuana magamba" kweli kuna uwezekanow wataweza? Na ukweli ni kuwa walipofika sasa hawawezi kurudi kwenye misingi ya Nyerere na Taifa letu; kwa sababu kurudia misingi hiyo ni kujishtaki katika historia.
kuna namna moja ttu ya kuwasaidia... kuendelea kuwakataa.
Maskini CCM!
Maskini Kikwete
Maskini Tanzania chini yao!
Dk. Slaa: Mtwara wamepuuzwa
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuomba hekima kwa Mwenyezi Mungu kutokana na matukio yanayotokea sasa nchini.
Alisema hali inayotokea sasa ni matokeo ya wananchi kupuuzwa na kutokusikilizwa katika suala zima la uwekezaji unaofanyika sehemu mbalimbali za nchi.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana katika kijiji cha Giroda Babati vijijini, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika ziara yake ya siku tisa ya ujenzi wa Chama mkoani Manyara.
Kabla ya kutoa kauli hiyo Dk. Slaa aliwaomba wananchi wasimame kwa muda wa dakika moja, kuomboleza vifo vilivyotokea mkoani Mtwara.
Aliongeza kuwa kuendelea kuwapuuza wananchi wa Mtwara ni kuendelea kucheza na jipu linalopaswa kutumbuliwa na kwamba njia sahihi ni kukaa na kuwasililiza wananchi katika uwekezaji na kufikia muafaka pasipo kutumia nguvu.
Alisema wanachotaka wananchi wa Mtwara ni kujua namna watakavyonufaika kwa kile alichoeleza kuwa katika uwekezaji wowote wanufaikaji wa kwanza wanapaswa kuwa wananchi.
Alisisitiza kuwa katika hali ya Mtwara kulihitajika busara za kawaida za kutatua msingi wa tatizo badala ya wananchi kupigwa mabomu, risasi na kisha kukamatwa.
“Ni jambo la aibu kuwapiga mabomu wananchi wanaodai kunufaika na rasilimali za nchi yao hapa kunahitajika elimu ya kuwafahamisha haki zao ni zipi na siyo mabomu,” alisema Slaa.
Thursday, May 23, 2013
Wabunge wasiwe watoro majimboni Mwao!
KATIKA hali isiyo ya kawaida nchini, baadhi ya wabunge wameyatelekeza majimbo yao kwa kutorudi kusikiliza kero za wananchi na kutimiza ahadi zao.
Imefikia baadhi ya wanasiasa wanadhani majimboni ni sehemu ya kuchota kura na kuwaacha wananchi waendelea kubaki kama walivyo kana kwamba wapo kisiwani kusiko na msaada, huku hawajui ni lini wataokolewa labda pale tu watakapofanya maamuzi magumu ya kuitosa.
Wananchi katika Majimbo mbalimbali nchini wamemekuwa wakilia na tabia ya wabunge wao waliowachagua ili wawawakilishe bungeni, kwa bahati mbaya baadhi yao wamekuwa wasaliti kwa wapiga kura wao, kutokana kuonekana mara chache kwenye majimbo yao.
Hali hiyo imewapelekea wakiwa wabunge hao wakiwa bungeni, hulipuka kusema mambo ambayo hawakuagizwa na wapiga kura, kitendo ambapo muda wao huishia kuwashukuru wake zao, kutukana matusi, sanasana kulala usingizi, bila kusemea kero za majimboni mwao.
Kutokana na wabunge kuasi majimboni kuongee na wapiga kura nini wakazungumze bungeni dhidi ya kero zinazowasibu, utashangaa wanabakia kusikiliza wapinzani wamepinga kitu gani ili waanze kuwashambulia, badala ya kuwatetea wapiga kura wao.
Uchunguzi ambao umefanywa na kubaini mapungufu kadhaa ya wawakiliishi hawa, wabunge karibu wote imebainika wanakwenda mara chache sana majimboni mwao, na wanaweza kwenda na wasifanye mikutano yoyote, jambo linalowaudhi wananchi.
Kuthibitisha malalamiko ya wapiga kura na wananchi wa baadhi ya majimbo, ukichunguza kwenye mahudhurio yao kwenye vikao vya DCC na RCC, wabunge hao ni nadra kuhudhuria kwenye vikao hivyo.
Mara kadhaa ukisoma kwenye mihutasari utaona labda ni mbunge mmoja tu alikuwepo, lakini wengine wote utakuta imeripotiwa ni udhuru tuuu, jambo ambalo linawakasirisha sana wapiga kura na wapenzi wa vyama husika.
Mwananchi mmoja wa Mvomero ambaye ni Kiongozi wa Chama kinachotawala (CCM) aliyeomba asitajwe jina lake kwa kuhofia kukemewa alichodai ni kukolimbwa kwa kudai haki alisema, ”Tumechoshwa na wabunge wanaojifanya wazaliwa wa wilaya na mikoa ya maeneo yetu, na baadaye wanahamishia makazi na shughuli zao Dar es Salaam.
“Kimsingi tunatafakari kwa umakini Udanganyifu huu na Usanii tunaofanyiwa na baadhi ya wabunge wetu, kuchota kura na kamwe tutaendelea kubaki kama tulivyo kama watu walio kwenye kisiwa na hatujui lini tutaokolewa labda pale watakapofanya maamuzi magumu ya kuitosa CCM mwaka 2015”.
Wakati wapiga kura wakiwalalamikia wabunge wasiochukua maoni yao na kuwatetea bungeni, Rais Dk. Jakaya Kikwete kwenye kikao chake na wabunge wa CCM Dodoma hivi karibuni, amekea tabia ya wabunge watoro wasiotembelea majimbo yao.
Katika kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma, Imefahamika Rais amekaririwa akisema baadhi ya wabunge wameyatelekeza majimbo yao kwa kutorudi kusikiliza kero za wananchi na kutimiza ahadi zao, kitendo ambacho ni hatari kwa wao kurudi kwenye majimbo yao na CCM.
Hivi karibuni bila ya kuuma uma maneno kwa Mkutano wa hadhara, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe amewachongea Wabunge wa Mkoa wa Tabora (CCM) kwa wananchi, akidai ni wasaliti kwa wapiga kura wao, ambapo baadhi ya wananchi walimuunga mkono.
Ni rai yangu Wabunge wa namna iliyoelezwa, wajikague wajitathimini, ili wasiwe watoro majimboni na kuwa Viwete, Bubu, Vipofu na wagumu wa kuwatetea wapiga kura wao, ingawa ni rahisi kudai posho zao, wanahatarisha uwakilishi wao 2015.
0715-933308
Subscribe to:
Posts (Atom)
.jpg)
(2)(2).jpg)


