Sunday, December 20, 2015

MKUTANO WA MWISHO WA UKAWA WA KUFUNGA KAMPENI YA UCHAGUZI MDOGO WA MASASI

Selemani Bungala (Bwege) wa Kilwa Kusini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) akihutubia maelfu na wakazi wa masasi jioni ya leo
Idadi kubwa ya wakazi wa jimbo la Masasi na Viunga vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika uwanja wa mti wa mwiba jimboni hapo katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge ndani ya Jimbo hilo la Masasi
Mbunge wa jimbo la Kinondoni Jijini Dar es salaam kutoka chama cha wananchi CUF ndani ya umoja wa vyama vya UKAWA Mh MAULID MTULIA akiwahutubia maefu wa wafuasi wa vyama hivyo katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge ndani ya jimbo la Masasi ambapo uchaguzi huo unafanyika kutokana na aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo EMANUEL MAKAIDI kufariki dunia wakati wa uchaguzi mkuu uliomalizika mwaka huu.
Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mh HAMIDU BOBANI akiwahutubia wakazi maelfu waliojitokeza katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa pia na Wabunge wote wa upinzani kutoka Lindi,na mtwara Pamoja na wabunge wa zanzibar pamoja na mbunge wa kindondoni Jijini Dar es salaam
Polisi wakifanya doria wakati wa mkutano  wa kufunga kampeni katika jimbo la masasi


Mbunge wa Jimbo la ndanda Mh CECIL MWAMBE akiwahutubia maelfu ya wafuasi wa vyama vya Ukawa katika mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo la masasi,Mkutano uliofanyika katika uwanja wa mti wa mwiba Jimboni humo

No comments:

Post a Comment