Saturday, December 19, 2015

Lissu awagalagaza wapinzani wake

JAJI wa mahakama kuu ya Dodoma jaji Seheni, ametupilia mbali maombi ya Jonathan Njau (CCM) ya kutaka apunguziwe gharama ya uendeshaji wa keshi ya kupinga uchaguzi nafasi ya ubunge dhidi ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu (Chadema). Anaandika Dany Tibason, Dodoma … (endelea).


Katika kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2015 Njau aliomba asitoe kiasi cha shilingi milioni 15 ambacho kipo kisheria kutokana na kutokuwa na hela kwa madai kuwa hela hizo ni nyingi na hawezi kuzipata kutokana na ukata alionao baada ya uchaguzi.

Akisikiliza kesi hiyo jaji Sheheni alisema haiwezekani kupunguza gharama hiyo kwani hipo kisheria.

Awali Lisssu aliweka pingamizi kwa madai kuwa maombi pamoja na viapo vyote vimekosewa na kuna kila sababu ya kupeleka fedha hizo ili kukithi matakwa ya kisheria.

Akizungumza nje ya Mahakama Lissu amesema: “Watu walileta maombi ya kusamehewa kulipa fedha za gharama za kesi sh milioni 15 yule bwana anayetishia wapiga kura wangu kuwa yeye ni bilionea alileta maombi ili asamehewe kwa madao ameishiwa ,sasa ameleta maombi na viapo vimekosewa na hajatimiza masharti ya kisheria.

“Kwa hiyo nilimwekea pingamizi kuwa maombi na viapo vilivyo letwa mahakamani havijafuata sheria na tukaomba yafutiliwe mbali na jaji ametukubalia kwa hiyo hakuna maombi hapa” amesema Lissu.

Amesema kutokana na kufutiliwa mbali maombi hayo sheria inaeleza kwamba isipopelekwa sh.milioni 15 kesi hakuna.

Lissu amesema kutokana na hali hiyo hakuna kesi ya msingi hakuna hadi hapo itakapokuwa imepelekwa fedha hiyo.

Lissu anasema kuwa Njau kamtuhumu kuwa aliwaonga viongozi wa dini, alinywesha watu pombe,alihonga mashuleni na kuwapiga wapiga kura.

Amesema tuhuma ambazo Lissu ametuhumiwa zinalenga kumzuia kufanya siasa kwa kipindi cha miaka 10. Hata hivyo alisema wakili Wasonga ambaye anamtetea mteja wake ambaye aligombea ubunge kupitia CCM alisha wahi kufanya makosa yale yale katika kesi ya mwaka 2010.

“Mwaka 2010 Wasonga alileta makosa yale yale yenye makosa yale yale kama haya ambayo yameletwa leo yenye makosa ambayo yamefutwa,” amesema.

MwanaHalisiOnline

No comments:

Post a Comment