Monday, June 22, 2015

Salum Mwalim awataka wanafunzi SEKOMU WASISALITI wajibu wao.


Na Mohamed Mtoi
Naibu katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar Salum Mwalim amewakumbusha vijana nchini hususani walio vyuo vikuu wajibu wao wa kusimamia kupatikana kwa uhuru wa pili wa nchi wenye lengo la kuwakomboa watanzania kutoka katika maisha magumu. Mwalim ameyasema hayo jana mjini Lushoto wakati akiongoza mahafali ya wanachama wa Chadema wanafunzi wa chuo kikuu cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU)- ambapo alikabidhi vyeti kwa wahitimu.

Mwalim amesema kuna ushawishi mkubwa unaofanywa na ccm kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ili wakubalike ikiwemo kumwaga fedha na ahadi za vyeo na ajira ili kuwapupambaza vijana kuondoka katika msitari wa harakati. Mwalim amewakumbusha vijana hao kuwa kila kizazi kina jukumu lake na kwamba kizazi cha baba wa taifa Mwl Julius Nyerere kilikuwa na jukumu la kuwakomboa watanzania kutoka mikononi mwa wakoloni na kwamba kazi ya kizazi cha sasa ni kuitafutia Tanzania uhuru wa pili.

Amewapongeza vijana hao wa SEKOMU kwa kusimamia na kunadi sera za Chadema na kuwapa changamoto ya kuwania nafasi za ubunge na udiwani kwenye uchaguzi mkuu ujao wa unaotarajiwa kufanyika oktoba 25, 2015.

Amewaambia vyeo, fedha na ajira nzuri watazipata na kuzifaidi kwa haki, heshima na amani baada ya ccm kung'oka madarakani tofauti na watakapokubali kupokea sasa kama rushwa ya kusailiti wajibu wao kwa taifa. Mwalim amesema serikali ya Ukawa itatatua changamoto zilizopo- elimu ya juu katika kipindi cha kwanza cha miaka mitano kwani niza kutengenezwa na serikali ya ccm kwa masilahi yao binafsi na si kweli kwamba hazina suluhisho la kudumu.

Naye mratibu wa kanda Taifa Mohamedi Mtoi ambaye ni mtia nia wa jimbo hilo (Lushoto mjini) amewaasa wahitimu hao wasiache kuendeleza harakati na kupigania haki za watanzania wengine katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu kwa kuwataka wawe chachu ya kuhamasisha watu wenye sifa ya kuandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura linalo endelea kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.

Amewaambia wana wajibu wa kujua ratiba za maeneo yao na kuhamasisha vijana na wazee kujiandikisha kwani ndio silaha pekee ya kuung'oa utawala wa serikali ya ccm ambayo imeshindwa kutimiza ahadi ya kuwaletea watanzania maisha bora na matokeo yake gharama za maisha zimepanda na mateso kwa watanzania yameongezeka kwa kukosa huduma za msingi za kijamii.

Mahafali hayo yamefanyika kwenye ukumbi wa hotel ya kakakuona na kuhudhuriwa na viongozi wa chama wa jimbo na wilaya ya Lushoto.

No comments:

Post a Comment