Saturday, June 20, 2015

MUSSA HASSAN ZUNGU APATA MPINZANI JIMBO LA ILALA

MUSLIM HASSANAL akizngumza na wanahabari kuhusu lengo lake kwa wana ilala.
MUSLIM HASSANAL akionyesha FORM ambayo tayari amekwishaijaza na kuirejesha leo

Mwanachama wa chama cha Democrasia na maendeleo Chadema jimbo la ilala Bwana MUSLIM HASSANAL leo ametangaza rasmi nia yake ya kumngoa katika kiti cha ubunge mbunge wa jimb o la ilala mh MUSA ZUNGU katika uchaguzi ujao mwishoni mwa mwaka huu.

Hayo ameyasema muda huu Jijini Dar es salaam wakati akirudisga Form ya kugombea ubunge katika jimbo hilo la ilala tukio lililofanyika katika ofisi za kanda za chama hicho Akizungumza na wanahabari mara baada ya kurejesha Form hiyo Bwana MUSLIM amesema kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa Jimbo la ilala linarudi katika hadhi yake ya kuwa jimbo la mfano katika majimbo yote ya Dar es salaam ukizngatia kuwa jimbo hilo ndilo linalobeba Jina la Dar es salaam kwa kuwa na ofisi mbalimbali na kubwa za serikali.

“Ukizngumzia uchafu Dar es salaam lazima uitaje ilala,ukigusia ubivu wa miundombinu lazima uitaje ilala,ukitaja wananchi kuishi kwa hali duni lazima uitaje ilala,sasa sisi kama chama tumeamua kuhakikisha kuwa hali hii inafutika na tutalirejesha jimbo la ILALA mikononi mwetu kama ukawa watanipa nafasi ya kugombea katika jimbo hilo”alisema mtia nia huyo anayeonekana kujiamini sana. kinondoni Jijini Dar es salaam.

Ameongeza kuwa ukimtizama unawezaa k,udhani yeye sio mtanzania ila kwa ufupi yeye ni mzaliwa wa Tanzania na maisha yake yote amekulia kariakoo,hivyo anajua matatizo ya wananchi wa ilala kwa ujumla,na amejipanga kuhakikisha kuwa anashirikiana na chama chake kwa kupitia ukawa kuwasaidia wananchi hao.

Bwana MUSLIM HASSANAL aliwahi kugombea ubunge katika jimbo la kigoma kaskazini uchaguzi uliopita lakini hakufanikiwa kupita ambapo DAVID KAFULILA wa NCCR-MAGEUZI alishinda,ambapo akizunguzimzia hilo amesema kuwa kigoma ndipo walipo babu zake na ndio maana aliwahi kugombea huko lakini kwa sasa anadhani ni muda wa kumuunga mkono KAFULILA kwani bado anastahili kuongoza jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment