Thursday, June 25, 2015

Chadema yakomba 300 toka CCM Kikombo, Chololo.

Na Bryceson Mathias, Kikombo Chamwino.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya Kikombo Wilaya ya Chamwino Dodoma, kimekomba Wanachama 300 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa Vijiji vya Kikombo na Chololo, huku kikimruhusu, Yona Kusaja, atangeze Nia ya kugombea Udiwani bila Mpinzani.

Katika Mikutano ya Watia Nia wa Udiwani na Ubunge iliyofanywa na Chadema nchini kote hivi karibuni; Katika Kata ya Kikombo, ilimalizika Chadema kikikomba na kuzoa Wanachama 200 toka Kijiji cha Kikombo, ambapo Kijiji cha Chololo walizoa Wanachama 100.

Mikutano hiyo, iliyofanywa na Kusaja ambaye 2010 anadai alichezewa rafu ya matokeo yake na Mashushu wa Serikali, amejigamba kuwa aliporwa haki ya Ushindi wa Udiwani wa Kata hiyo kwa hila, hivyo amewashukuru Wanachama kumwani na kutaka asiwe na Mpinzani wa Chadema.

“Najua Sisi wote tulipigika na Uongozi wa Kata uliopo madarakani, ila nashukuru wananchi wamebaini na kuelewa makosa yaliyofanyika kwa hila, na ndiyo maana Ishara ya kuonesha hasira yao, wamefanya kweli kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na kushinda kwa Kishindo.

“Naomba Ushindi, na Imani kwangu, vitumike kufanyia maamuzi Magumu kwenye Uchaguzi Oktoba 25, Mwaka huu, kwa kuhakikisha tunang’oa Mizizi ya CCM na Maangamizi ya Uporwaji wa Uchumi wa Wananchi wa Kikombo, walionyanyaswa na Kuteswa kwa Miaka Mitano.alisema Kusaja.

Kata ya Kikombo, ina Mitaa Mitatu, Kikombo Makulu, Mnadani na Chololo; Lakini katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopita, Chadema kilishinda Mitaa Miwili ya Kikombo Makulu na Mnadani, ambapo CCM iliambulia Kiti Kimoja, ambapo Wana CCM 100 wametimkia Chadema.

Wiki ijayo, Viongozi wa Chadema Taifa, wanataraji kufanya Mkutano Mkubwa katika Kata hiyo, ambapo Viongozi wa Kanda, Mkoa wa Dodoma na Wilaya ya Chamwino, watahudhuria katika Mkutano huo, ambapo kuna taarifa Wana CCM wengine warejesha Kadi na Kujiunga na Chadema.

No comments:

Post a Comment