Thursday, June 25, 2015

Viongozi wa Dini; “Kikwete Simamisha Muswada wa Habari”

Na Bryceson Mathias, Dodoma
WAJUMBE wa 205 wa Kamati ya Maadili ya Amani na Haki ya Jamii ya Viongozi wa Dini nchini, wameitaka Serikali kusimamisha Muswada wa Uhuru wa kupata Habari kujadiliwa bungeni kwa madai, unawanyima haki Watanzania kupata habari, na haukustahili kuibuliwa wakati wa Uchaguzi.

Kamati hiyo imemuomba Rais, Jakaya Kikwete, ikimtaka akumbuke Kauli yake mwenyewe ya mwaka 2001 akihamasisha wadau wa habari, aliposema, kama Wananchi watakosa habari ndani ya mfumo wetu nchini, watazitafuta nje.

Akikiri kuwa na Kikao cha Viongozi hao Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekoste Tanzania, William Mwamalanga, alisema mbali ya Kumtaka Kikwete asitishe Muswada huo, pia wanapinga Njama zozote zilizojificha nnyuma ya Muswada huo.

Mbali ya kusema Viongozi hao kuunga wanaunga Mkono Tamko la Wanachama wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT) la kutaka Muswada huo usingeenda kujadiliwa bungeni, Mwamalanga amedai, Muswada huo kwa Wadau ni kama ‘Petroli kwenye Moto’.

Katika Kikao hicho Wandishi hawakuruhusiwa kwa madai wataruhusiwa siku ya Mwisho ambapo Viongozi hao watataka Umma katika siku ya siku ya Nne (4) uhabarishwe, ingawa Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kunasa kilichozungumzwa miongozi mwa Viongozi wa Dini na kumhoji Askofu Mwamalanga kama ni kweli.

Miongoni mwa Maazimio Saba yaliyoazimiwa na Mashekhe na Ma-Askofu hao ambao ni Wajumbe kutoka kila Mkoa, ni pamoja na kuupinga Muswada huo na Kuiunga Mkono MOAT na Wadau wa habari katika Kilio chao.

Yaliyokuwemo ni ‘ Uhuru wa Habari si wa Vyombo vya habari, Wandishi na Wamiliki pekee yao, bali ni wa Wananchi, hivyo haikuwa haki kupelekwa bungeni wakati wa Uchaguzi kwani ulitakiwa upitiwe na wenye Ueledi ili usiwabinye wadau hao kupata habari.

Wamedai, Muswada huo utawafanya Wadau wa Habari na Wananchi, wawachukie wabunge wao, hasa kutokana na ukweli kwamba, Mchango wa Vyombo vya Habari, umechangia kwa asilimia 81% kufichua uharifu wa Rushwa, Ufisadi na kuliletea Taifa Maendeleo ya Kiuchumi, Kisiasa na Kijamii.


Wamesema, Vyombo vya Habari na Wanahabari vimekuwa ndiyo sehemu pekee ya Kimbilio la Wananchi wanyonge katika kupata Haki zao kwa haraka kuliko Mihimili mingine yoyote, hivyo ni wajibu Muswada huo urudishwe kwao ili wenye Ueledi na Taaluma hiyo waujadili.


Wamedai wanapinga Njama zozote zilizojificha nyuma ya Muswada huo, kwa kupelekwa kwa Muswada kwa hati dharula, kunadhihirisha kilichoko nyuma ya Pazia hilo, na kama umelenga kuwanyima Wananchi taarifa za Uchaguzi, basi wahusika wameweka Petroli kwenye Moto.

Aidha Mwisho walisema, Kuchezea Tasinia ya Habari na Uhuru wake ni sawasawa na kuchezea Petroli kwenye Moto, hivyo wanamuomba Rais Kikwete kusitisha Muswada huo na kuwasikiliza Wadau wake, kwa sababu Kuwaburuza ni kutowatendea Haki, isipokuwa kuchochea Vurugu.

No comments:

Post a Comment