Friday, June 19, 2015

CHADEMA; Wananchi! “Kama na Sindano tunaagiza Nje”, Ipumzisheni CCM!.

Na Bryceson Mathias Morogoro.
MTIA Nia wa Udiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kata ya Kihonda Maghorofani; Msomi, Elizeus Rwegasira, amesema kama Wananchi wanashuhudia jinsi Serikali yao ianvyonunua hata Sindano, Leso na Njiti za kuchokolea Meno nje ya nchi, basi Waisaidie Chadema kukipumzisha Chama cha Mapinduzi (CCM).

Rwegasira alisema hayo jana Kihonda, baada ya Tume ya Uchaguzi (NEC) Juni 16, Mwaka huu, kukwama kuanza kuandikisha Wananchi wa Mkoa wa Morogoro na Wilaya zake, kwa madai ya kukosa Wino (Cartridge) na Vifaa vingine; huku wakjinasifu kama vitapatikana, Uandikishaji utaanza baada ya siku tatu.

“Kilichoua Viwanda na bidhaa za Kilimo na Ngozi, (Katani, Chai na Pamba), nz ajira ya Vijana, ni hao hao ambao sasa wanahujumu Uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Kiharamia, ili watu wasipata Haki ya Kuchagua Viongozi makini, wataorejesha Viwanda na Kuongeza Vingine.

“Hata wanaoridhia kuongezwa kwa bei ya Mafuta ya Taa yanayotumika na Walalahoi vijijini wakiwa hawana hata uwezo wa kuyanunua, isipokuwa wanachofanya ni kuharibu Mazingiraa na kuendelea kutumia Nyasi na Vijinga kupata Mwanga ili watoto wao wajisomee”.alisema Rwegasira.

Alisema, Wananchi; jueni Wanaotaka Mafuta yaongezwe bei, wana Maslahi binafsi; Hao ndio Wanasiasa wenye Meli, Mabasi, Malori, wanaotaka Reli ife, wao wafaidike, Viwanda Vife, bidhaa za Kilimo na Ngozi za Walalahoi zikose Soko, ili wao wazinunue kwa bei Ndogo, wakauze Nje kwa bei kubwa.

Ndugu zangu, “Mnapoona hayo na Kutambua, hakikisheni mnajiandikisha, Hata kwa Kukaa katika Vituo vya Uandikishaji hadi asubuhi, ili wakitaka kuwanyima haki ya kujiandikisha wakiwa na lengo la kuzuia Mafuriko ya Ukombozi kupitia Msukumo wa CCM, Mgangamale”.alisema Rwegasira.

Amewasisitiza Wananchi wa Kata yake ya Maghorofani na Mtaa anaouongoza wa Maghofani ‘A’ ambao yeye ni Mwenyekiti aliyeshinda kwa Tiketi ya Chadema na nchini kote, wasikubali Uongo na Usanii wa kwamba hakuna Wino, wakazmuz kurudi nyumbani, bila kujizndikisha, hiyo ni mbinu ya kuwakatisha tamaa wasijiandikishe siku ziishe.

Hivi karibuni, Utawala wa Mkoa wa Morogoro, uliviandikia Vyama vya Siasa, vikiwajulisha viwaandae watu wao kushiriki Uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kuanzia Juni 16-Julai 16, mwaka huu; Jambo ambalo zoezi hilo lilikwama kwa kukosa Wino na Vifaa vingine.

No comments:

Post a Comment