Friday, June 19, 2015

Chadema Mvomero; NEC inafanya Zoezi la BVR kwa Zimamoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mvomero Wallace Karia


‘Zoezi la Uandikishaji lakwama kwa kukosa Wino’!.

Na Bryceson Mathias, Mvomero Morogoro.
KATIBU Mwenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ramadhani Mrisho, ameuponda Utendaji wa Tume ya Uchaguzi (NEC) akidai, Kitendo cha kushindwa kuanza kuandikisha Wapiga Kura kwa mfumo wa Biometric Voters Registration ((BVR) 16/6/2015, inaonesha inafanya kazi hiyo kwa Zimamoto.

Kauli Mrisho kuiponda NEC na Watendaji wake kuwa si lolote wala chochote, linatokana na Zoezi hilo lililotarajiwa kuanza katika Jimbo lake la Mvomero Juni 16 hadi Julai 16 mwaka huu, kukwama kufanyika kutokana na kukosekana kwa kitu kidogo tu, ati ‘Wino’.

“Serikali kupitia Ofisi ya Utawala wa Mkoa wa Morogoro iliviarifu Vyama kwa Barua kwamba, Viaandae Mawakala wao kama makubaliano yalivyofanywa na Vyama hivyo, lakini tunaambiwa Mashine zaidi ya 80 zimefika kwa Mshangao tunataarifiwa Wino hakuna, si Usanii huu?

“Hii inadhihirisha jinsi ambavyo NEC haijajipanga, na kwamba inafanya Zoezi hili kwa Shinikizo la Mtindo wa Zimamoto. Kwa nini Mashine ziwepo halafu Wino ukosekane kama wana Mpango Kazi wa kufahamu Idadi ya watu fulani wanatumia Wino Kiasi gani? Alisema Mrisho.

Mrisho alisema kuwa, Kutokana na hali hiyo, imefahamika kwamba, zoezi hilo lingesababisha siku tatu za Uandishaji 16-19 lisimame huku wino huo ukisubiriwa, ambapo pia imefahamika kwamba, siku tatu zitakazopotea zitaongezwa ili kufidia uzembe wa makosa hayo.

Wakizungumza na Tanzania Daaima kwa nyakati tofauti, Wananchi na Viongozi wa Vyama Vyote vya Siasa Mvomero, wakiwemo Madiwani, Wenyeviti na Watendaji wa Kata, Vjijiji, Vitongoji, Wameishushia Lungu la lawama (NEC) wakidai, kukosekana kwa Wino, inaonesha watendaji hao wasivyo wajibika, kwa kudhani kazi hiyo ni ya Mzaha.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mvomero,Wallace Karia alipotakiwa kutoa majibu Wino huo utapatikana lini kuwaondoa wasiwasi wananchi, alipopigiwa simu yake ya Kiganjani 0754-339995 atoe ufafanuzi huo, simu yake ililia bila majibu na baadaye alijibu kwa SMS ‘I’am Driving’.

No comments:

Post a Comment