Sunday, March 16, 2014

MATUKIO KUTOKA IRINGA KWENYE HITIMISHO LA UCHAGUZI WA UBUNGE

Mh Freeman Mbowe akimjulia hali na kumsikiliza Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili akiwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, ambapo mbunge huyo alimwelezea kiongozi huyo namna alivyotekwa, kuteswa na watu aliodai kuwa ni vijana wa kikosi cha ulinzi cha Chama Ch Mapinduzi (CCM), Green Guard.

Mwenyekiti Mh Freeman Mbowe akisikiliza maelezo kutoka kwa Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee, namna ambavyo Mbunge Rose Kamili alikuwa akiendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo.


Mwenyekiti Mh Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari juu ya tukio la kutekwa na kuteswa kwa Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili lililotokea juzi usiku katika Kijiji cha Kitawaya, Kaa ya Luhota, jimboni Kalenga, wakati alipokuwa akizungumza na mawakala wa CHADEMA, ambapo imedaiwa kitendo hicho kilifanywa na vijana wa ulinzi wa CCM.


Mgombea wa CHADEMA, Grace Tendega Mvanda akiwa na Kampeni Meneja wake, Godbless Lema walipokuwa wakizunguka katika ameneo mbalimbali kuangalia shughuli ya upiogaji kura vituoni ilivyokuwa ikiendelea jana.



1 comment:

  1. Ya Kalenga yamepita sasa tuelezeni ya Chalinze???Hivi huyu kijana wa Kimasai mmemtosa kabisaaaaaaaa au ndo mmekata tamaa baada ya kichapo cha chalinze.Sisa si mdomo mtupu ni vitendo,acheni blaablaa fanyeni kazi mliyoomba kwa wananchi nayo ni kuwatumikia.

    ReplyDelete