MADIWANI wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Mvomero, wakishambulia Chama cha
Mapinduzi (CMM) kwa kushindwa kuwatatulia wananchi kero zao na kudai badala
yake viongozi wake wamekuwa wakiwafanya watumwa katika nchi yao.
Hayo yalisemwa na
Madiwani hao Katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Januari 13, Kijiji cha
Kigugu Kata Sungaji, moja ya eneo lililokuwa na Mapigano ya Wakulima na
Wafugaji, wilayani Mvomero, ambapo wanachama 20 wa CCM walivua Magamba na kuvaa
Magwanda.
Wakiongozwa na
Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema Morogoro na Diwani wa Gairo Mjini, Dunstan
Mwendi, alisema, Wananchi wa Kigugu wasidanganyika tena na Ubwabwa, Kanga,
Tisheti, Skafu, bali wawachague Viongozi wa Chadema tangu Balozi hadi Mbunge
ili wawaondolee kero zilizowatesa miaka Mitano.
“Mlidanganyika
kutochagua, Wenyeviti wa Vitongoji, Mitaa, Vijiji, Diwani wa Kata, Jairos
Msigwa, na Mbunge Matokeo Wardern, waliogombea kwa tiketi ya Chadema, kwa miaka
Mitano cha moto mmekiona, kero zipo pale pale na ardhi mmeporwa”.alisema Mwendi
akitaka wasifanye kosa hilo chaguzi za serikali za mitaa.
Diwani wa Kata ya
Nyandira, Luanda Zengwe, alisema, wananchi wa Kigugu wasikubali kuishi maisha
ya Panzi ya kuliwa na Kunguru kila siku, bali wakatae na wabadilike kwa
kukichagua Chadema kwenye chaguzi za Serikali Mitaa, ambacho hata walipowekwa
ndani kiwawekea dhamana.
Kwa Upande wake Diwani
Kata ya Mtibwa, Luka Mwakambaya, aliwaambia wananchi wa Kigugu waige Ujasiri wa
wananchi wake (Mtibwa), ambapo wakidhurumiwa haki zao na Mwekezaji wa
Kiwanda,anakesha nao Langoni kwa Mwekezaji hadi haki ipatine.
Aidha katika Mkutano huo Matawi Mashina matatu
ya Chadema yalifunguliwa, ili kuwawezesha wananchi kwenda kutoa kero katika
ofisi hizo ziweze kushughulikiwa, ambao wanachama waliovua magamba na kuvaa Magwanda walisema,
waajuta kuchelewa maamuzi hayo,
hongereni madiwani kwa kutambua mchango wa CHADEMA katika kuimarisha utu wa wa watanzania kwa ujumla, tuipende siku zote nchi yetu na tukipende chama chenye mwelekeo chanya,,CHADEMA
ReplyDelete