Monday, April 30, 2012

TUSIPUUZE WOSIA WA MWALIMU NYERERE - LETICIA NYERERE MP

Ni jambo la kusikitisha kuona nchi yetu inatafunwa wazi wazi.Nasikitika kusema kuwa nadhani baadhi ya watanzania tulipuuza wosia wa baba yetu, baba wa taifa Mwalimu Julius K. Nyerere. Nadhani laana zake zimeanza rasmi. Baada ya kumfahamu na kuishi na mwalimu kwa takribani miaka 12 kama mkwe wake, nilitambua nguvu pekee ya mwalimu ambayo haiazimishwi,Nasikitika baadhi yetu tumeshindwa kumuenzi baba wa taifa na ninachokiona mbele yangu ni laana za mwalimu baada ya kupuuza wosia wake. Watanzania tusishangae yote yanayotusibu, kuna sababu, tupige magoti ,tutubu tumweke mwalimu kwenye maombi yetu, pengine mwenyezi Mungu atatusamehe!.Leticia Nyerere(MP) 

No comments:

Post a Comment