Sunday, April 29, 2012

Hukumu ya kupinga ubunge sumbawanga mjini

Kesho tar 30/04/2012 ndo siku ya hukumu ya kesi kupinga ubunge wa bw Aesh Hilaly Khalfan Wa Sumbawanga mjini, kesi hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA bw Noberth Yamsebo akilalamikia ugubikwaji wa uvunjifu wa sheria ya uchaguzi uliofanywa na bw Aeshi kwa kujihusisha na rushwa na uchakachuzi wa matokeo uliofanywa na msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo bi Sylvia Siriwa. 

Hali ni shwari hapa Sumbawanga, askari wamemwagwa kwa wingi sana. Kila upande kwa maana walalamikaji CHADEMA na walalamikiwa CCM wanajigamba kwa kuibuka kidedea hapo kesho. Wenye kujihakikishia zaidi ni wanaccm kwani wanasema mahakama na dola ni ccm na hivyo wao hawana wasi wasi kwani mbunge wao lazima ashinde, waandishi wa habari nao wamejiandaa vilivyo kuhakikisha wanaripoti vilivyo yote yatakayojili mahakamani, na hasa ikizingatiwa kuwa waandishi wengi wako upande wa bw Aeshi na ndo maana walishindwa kuripoti namna kesi ilivyoendeshwa hadi ushahidi ulivyofungwa kwani kwa kiasi kubwa ilionekana kwao baadhi ya waandishi wa habari ni udhalilishaji kwa bw Aeshi na kwa baadhi ni wale waandishi njaa ambao kwao hawawezi kuripoti bila fedha na ndo maana hiyo kesho bw Aeshi akishida kama wanavyotegemea watajipendekeza kwake na kupata chochote.

Zaidi tu ni kuwa ujumbe unasambazwa na watu wasiojurikana kwa njia ya sms kuwa Tahadhari: Usiende mahakamani J3. Kutakuwa na; Mbunge ni yule yule, askari wanafanya maandalizi, wadai wamelazimishwa ingawa hawapendi, jaji apewa ulinzi makali na jeshi la polisi”

Taarifa za uhakika ni kuwa ujumbe huo polisi wameupata na Jana kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa aliwaita baadhi ya viongozi wa CHADEMA mkoa wa Rukwa akiwepo katibu mh Ozemu Chapita na kuwaeleza kuwa ujumbe huo waupuuze kwani polisi haijihusishi na wala haitakuja jihusisha na siasa za Sumbawanga, na kuhusu askari wengi waliomwagwa hivi karibuni,kamanda huyo alisema hao ni askari wapya wako mbioni kupelekwa mkoa mpya wa Katavi kama vituo vyao vipya vya kazi walivyopangiwa na kuwa muda wowote wataondoka, mwishowe aliwaasa viongozi hao wa CDM wawahamasishe wapenzi na wanachama wao wajitokeze kwa wingi na wasiwe na hofu na usalama wao, zaidi ya yote aliwaahidi kutoa hata gari kwa ajili ya kuwatangazia wananchi kupuuza uzushi huo wa ujumbe uliosambazwa.



CHANZO - JF

No comments:

Post a Comment