Monday, December 21, 2015

TUPAMBANE KUTETEA HAKI YA MKISI NA WATU WA VWAWA.


Malisa GJ

Naandika haya nikiwa na uchungu mwingi nafsini. Kuna mambo yanayofanywa na serikali ya CCM yanatia hasira, yanaudhi, yanakatisha tamaa. Naomba nitumie fursa hii kumshauri Rais Magufuli kuwa akiendelea kukaa kimya kwenye mambo haya wananchi watapoteza hata ile imani kidogo waliyoanza kuionesha kwake.

Vitendo vya ukiukwaji wa wazi wa demokrasia ktk chaguzi mbalimbali ni mambo ya kawaida sana kwa viongozi wa CCM. Kuanzia uchaguzi mkuu hadi chaguzi za Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri tumeona namna CCM wanavyotumia nguvu kubwa kupora madaraka.

Jambo kubwa nililojifunza ktk uchaguzi huu ni kuwa ili uweze kuishinda CCM inabidi ushinde kwa kura nyingi sana. Ukishinda kwa tofauti ya kura chache ujue umeumia. Hivyo ndivyo ilivyotokea kwa rafiki yangu Fanueli Mkisi MBUNGE HALALI wa jimbo la Vwawa.

Mimi na vijana wenzangu wa CHADEMA tulifanya ziara nchi nzima tukinadi wagombea Ubunge, Udiwani na Rais ktk majimbo 19 nchini. Kati ya wagombea 19 wa Ubunge tuliowanadi, 16 walishinda kwa kishindo na watatu hawakutangazwa washindi japo kiuhalisia walishinda. Mmojawapo kati ya hao watatu ni Mhe.Fanuel Mkisi Mbunge halali wa Vwawa.

Moja ya majimbo ambayo nilijua tutashinda mapema sana ni pamoja na jimbo la Vwawa kwa Mkisi. Na ndivyo ilivyotokea. Katika vituo vyote vya kupigia kura Mkidi alikua anaongoza kwa kura nyingi sana dhidi ya Japhet Hasunga wa CCM. Hata fomu za matokeo walizosaini mawakala zinsonesha hivyo.

Kwa hiyo hata kabla matokeo rasmi hayajatangazwa wananchi wa Vwawa walikua wameshaanza kushangilia barabarani na maeneo mengine ya wazi. Lakini katika hali isiyotarajiwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbozi ambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi akatangaza kuwa Japhet Hasunga (CCM) alishinda kwa kupata kura 36,705 dhidi ya Fanuel Mkisi (CHADEMA) kura 35,400. Tofauti ya kura 1,200.

Huu ulikua wizi wa mchana kweupe na wananchi wa Vwawa hawakua tayari kuuvumilia. Hivyo wakafunga barabara na kushinikiza mshindi halali (Mkisi) atangazwe. Lakini Polisi wakaishia kuwapiga mabomu na wakamsaidia Mkurugenzi kutoroka baada ya kutangaza matokeo hayo "feki".

Zipo taarifa kuwa Mkurugenzi huyo alipewa maagizo kuwa ahakikishe anamtangaza Hasunga kuwa Mshindi wa Vwawa kwa kuwa jimbo pacha la Mbozi tayari CCM walikwishapoteza.

Taarifa nyingine zinadai kuwa Ofisi ya Mkoa ilipewa maagizo kuwa ihakikishe CCM wanashinda zaidi ya nusu ya maJimbo ya mkoa Mbeya ili kupunguza nguvu ya upinzani. Ndio maana majimbo mengi CCM waliyotangazwa washindi wameshinda kwa tofauti ya kura chache sana. Hii ni dalili ya wazi kuwa hawakushinda kihalali.

Kwa sababu mgombea wa CCM akikushinda kwa kura moja anandikiwa 10. Ndio maana Lowassa alisema njia pekee ya kuishinda CCM kwa Katiba ya sasa ni kupata kura nyingi hadi washindwe kuiba. Yani wakiiba waone aibu. Kwa mfano ukipata kura 20,000 na mgombea wa CCM akapata kura 350 hapo anaibaje? Lakini ukipata kura 20,000 na CCM 19,000 ujue hapo atakayetangazwa mshindi ni CCM. Hivyo ndivyo Tume ya Uchaguzi isivyoheshimu demokrasia ya watu wake.

Kwahiyo Mkisi alishinda kwa zaidi ya kura 3000 lakini AKAPORWA USHINDI na Hasunga wa CCM akatangazwa mshindi. Karatasi za matokeo zilizosainiwa na mawakala zinaonesha Mkisi ndiye mshindi, karatasi zilizobandikwa nje ya vituo zinaonesha Mkisi ndiye Mshindi. Masanduku ya kura yanaonesha Mkisi ndiye Mshindi. Sasa Mbona ametangazwa mwingine? Haya ni maswali ambayo kila mpenda demokrasia anajiuliza.

Lakini kwa kuwa vipo vyombo vya kudai haki, Mkisi akaamua kwenda Mahakamani kudai haki yake. Akafungua Shauri Mahakama kuu kanda ya Mbeya akiwa na Jopo la Mawakili wanaomtetea akiambatanisha vielelezo vyote muhimu vinavyoonesha kuwa yeye ni Mshindi halali wa ubunge jimbo la Vwawa.

Lakini ktk hali ya kusikitisha Mahakama nayo inaonekana kutaka kuzuia haki ya Mkisi na wananchi wa Vwawa. Ktk hali isiyotsrajiwa Mahakama hiyo imeweka gharama kubwa sana za kusikiliza kesi hiyo (Cost for Security) kinyume na maombi ya mlalamikaji (Mkisi).

Mkisi aliomba Cost for Security iwe Tsh. Milioni 3 kama ambavyo wagombea wengine wamefanyiwa. Lakini Mahakama imekataa ombi lake na kumtaka alipe Tsh. Milioni 9 ndani ya siku 14 ili kesi yake iweze kusikilizwa.

Hizi ni dalili za wazi kuwa Mahakama imetumika kisiasa. Haiwezekami wagombea wengine watozwe Mil.3 then Mkisi atozwe Mil.9. Bila shaka Mahakama imetoa maagizo haya baada ya kuona kuwa wakitaja fedha ndogo Mkisi atazilipa na kesi yake itasikilizwa na ATASHINDA.

Kwa hiyo njia rahisi ya kumnyang'anya HAKI yake ni kumtajia kiasi kikubwa cha pesa ili ashindwe kulipa na hivyo kesi hiyo itupiliwe mbali. Hiki ni kiwango cha juu kabisa cha ukiukwaji wa misingi ya utu ktk mchakato wa demokrasia.

Nimezungumza na rafiki yangu Mkisi leo amesema hadi sasa amefanikiwa kupata Mil.4.7 tu. Ikumbukwe deadline ni jumanne ya tarehe 22 mwezi huu, na bado mil.4.3 kufikisha Mil.9 zinazohitajika na Mahakama.

Nichukue fursa hii kwa moyo wa unyenyekevu kabisa niwaombe ndugu jamaa na marafiki watakaoguswa kutoa chochote kumsaidia Mkisi afikishe kiasi hicho kinachohitajika na Mahakama ili kesi yake iweze kusikilizwa.

Nina uhakika kuwa kesi hii ikisikilizwa Mkisi atashinda na atatangazwa kuwa MBUNGE HALALI WA VWAWA.

Biblia inasema katika kitabu cha Mithali 10:3 kuwa "BWANA hataiacha nafsi ya mwenye haki ife na njaa; Bali tamaa ya mtu mwovu huisukumia mbali."

Kwa scenario ya Vwawa "mwenye haki" ni Mkisi na "mtu mwovu" ni Hasunga. Tusiiache nafsi ya Mkisi ikaangamia bali tuisukumie mbali tamaa ya mtu mwovu (Hasunga). Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumefanya kazi ya kitume na thawabu yake ni kubwa.

Pia nitoe wito kwa Wabunge wote wa Mkoa wa Mbeya washikamane kuwasaidia kina Mkisi na wengine wanaodai haki zao Mahakamani baada ya kuchakachuliwa. Joseph Mbilinyi (Sugu), Pascal Haonga, Silinde Ernest David, Frank Mwakanjoka, yangu Sophia Hebron na wengine naomba muwashike mkono kina Mkisi.

Kwa atakayeguswa na kupenda kuchangia chochote ili kuhakikisha haki ya Mkisi na watu wa Vwawa haipotei atume mchango wake moja kwa moja kwa Fanuel Mkisi kupitia namba 0766800090.

Kumbuka kesi imepangwa kusikilizwa jumanne tar.22, this means tuna siku moja tu kutafuta mil.4.3 ili kutimia mil.9 zinazohitajika. Otherwise HAKI ya watu wa Vwawa itakua imepotea.

Asanteni sana na Mungu awabariki,
Malisa GJ.!

No comments:

Post a Comment