Tuesday, December 15, 2015

GODBLESS LEMA AREJEA BUNGENI

Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amechaguliwa tena kwa mara ya pili kuongoza Jimbo la Arusha Mjini.

Akimtangaza Mbunge huyo, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arusha Mjini, Juma Idd alisema Lema ameshinda kwa kura 68,848 sawa na asilimia 65.7.

Alisema mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Philemon Mollel (Monban) amepata kura 35,607 sawa na asilimia 34 huku mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) Zuberi (849),Navoi Mollel wa (ACT) 342 sawa na asilimia 0.3 huku chama cha NRA (43).

Alisema Idadi ya wapigakura ni 317,814 ,waliojitokeza ni 105,800 sawa na asilimia 32.83 huku kura halali zikiwa ni 104,353 na zilizoharibika 1447.

No comments:

Post a Comment