Sunday, December 13, 2015

Fredrick Sumaye Atangaza Rasmi kuwa Mwanachama wa Chadema.........Akabidhiwa Kadi na Mbowe

Waziri mkuu wa awamu ya tatu Mh.Fredirick Sumaye jana alitangaza rasmi kujiunga na chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) na akakabidhiwa kadi na Mwenyekiti wa chama hicho Mh.Freeman Mbowe.

Sumaye ambaye wakati wa uchaguzi alitangaza kujiondoa CCM na kudai kuwa anaunga mkono mageuzi yanayofanywa na vyama vinavyounda katiba ya wananchi (UKAWA) bila kuweka wazi kuwa yuko kwenye chama kipi kati ya hivyo amesema sasa ameamua kujiunga na CHADEMA.


Akizungumza katika mkutano wa kufunga kampeni za ubunge wa jimbo la Arusha kwa chama cha CHADEMA uliofanyika kata ya Baraa, Sumaye alisema anataka kuungana na wanamageuzi wenzake katika kuendeleza harakati za mabadiliko hapa nchini ambazo bado zinaendelea.


Akizungumza baada ya kumkabidhi kadi Mwenyekiti wa chama hicho Mh.Freeman Mbowe alisema chadema na vyama washirika wa UKAWA bado viko imara na vimeendelea kuimarika na kwamba licha ya kudhulumiwa ushindi azma yao ya kuleta ukombozi nchini iko pale pale.


Awali aliyekluwa mgombea uras wa CHADEMA akiwakilisha vyama vya umoja wa katiba ya wananchi ukawa Mh.Edward Lowassa ameendelea kuwataka watanzania wanaounga mkono mabadiliko kuwa watulivu na kwamba kwa vile wana dhamira ya dhati ya kuyaona mabadiliko hakuna kukata tamaa kwani bado kuna fursa yakufikiwa kwa malengo yao .

No comments:

Post a Comment