Sunday, December 27, 2015

DIWANI WA CHADEMA AKATAA KUPOKEA POSHO ZA VIKAO

Diwani wa kata ya Gangilonga, Iringa Mjini kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Daddy Igogo amesema hatapokea posho za vikao vyote vya baraza la madiwani katika kipindi chake cha miaka mitano na badala yake ametaka zitumike kuwasaidia watoto wanaoshi katika mazingira magumu katika kata yake.

Diwani huyo mdogo kuliko madiwani wote wa halimashauri hiyo ambaye pia ni Mwalimu katika Chuo Kikuu cha Ruaha, Iringa anakuwa diwani wa kwanza nchini kukataa posho hizo huku baada ya Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu (CCM) naye kukataa kupokea posho kama hizo katika kipindi chote atakachokuwa mbunge wa jimbo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya kata ya Gangilonga Igogo alisema kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo ili kusaidia yatima na kuunga mkono ilani ya chama chake ya uchaguzi wa 2010 na 2015 ya kukataa posho ya vikao na kwamba ameshamuandikia mkurugenzi barua inayompa maelekezo ya wapi posho hizo zipelekwe.

Igogo alisema kuwa posho ya vikao ni ugonjwa wa ufisadi unaolitafuna taifa kila kukicha hususani kwa watendaji wa mashirika ya umma ,watendaji wa serekali kuu huu na kumpongeza Raisi John Magufuli kwa kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa fedha nyingi zaidi zinaelekezwa katika miradi ya maendeleo.

Alisema posho za wabunge zinalingana na bajeti ya sensa ambapo Taifa lilikwenda kukopa baadhi ya fedha ili kuendeshea zoezi hilo huku wastani wa posho kwa za madiwani na watendaji katika manispaa ya Iringa kwa mwaka zinauwezo wa kusomesha zaidi ya wanafunzi 400 wa shule za sekondari kwa ada ya shilingi eflu 20,000 kwa kila mmoja na fedha zikabaki

Hata hivyo Igogo aliwaomba madiwani wa chama chake na mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Piter Msigwa na wabunge wote wa viti maalumu kuwa sehemu ya kupinga uendelezwaji wa posho zisizo za msingi ili kuonyesha dhamira ya dhati katika kuwatumikia watanzania

Katika vhatua nyingine Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Wilaya ya Iringa mjini ambaye pia ni diwani wa kata ya Mivinjeni Frank Nyalusi amesema uamuzi aliochukua diwani huyo ni mzuri na ni maamuzi yake ila yeye hana mpango wa kugomea kuchukua posho hizo.

No comments:

Post a Comment