Thursday, August 27, 2015

Pingamizi la Mgombea wa CCM dhidi ya Chadema, latupiliwa mbali.

Na Bryceson Mathias, Mvomero-Morogoro.
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Sadiq Murad, dhidi ya Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Osward Mlay, wa Jimbo la Mvomero, Morogoro.

Akizungumza na Tanzania Daima, Mchungaji Mlay amekiri kuwekewa Pingamizi na Murad aktilia shaka Jina a Elimu yake, ambapo Mchungaji Mlay amesemaalmelijibu na limetupiliwa Mbali na anaendelea na Maandalizi ya kufungua Kampeni.

“Ni kweli niliwekewa Pingamizi na Mgombea Mwenzangu (Murad) wa CCM, lakini nadhani alikosa Uelewa, lakini nimelijibu Pingamizi lake na limetupiliwa mbali, na sasa najiandaa kwenda Morogoro kwa maandalizi ya Kampeni.

“Naomba niombeani, kimsingi hatuna muda wa kujadiliana na Watu ambao, Mungu amemwinua Musa aende kwa Farao, awatoa Watu waende nchi ya Maziwa na Asali, amemwinua Yusuf, akaandae Chakula kwa Miaka Saba ya Njaa inayokuja, halafu mtu anazuiamia, anazuia! Tusimkubali”.alisema Mlay”.

Chma kimenichagua nipeperushe Bendera ya Chadema, kwa hiyo katika hili, Wananchi na Wanachama wenye Uchungu wa Mateso waliyofanyiwa na CCM kwa Miaka 50 ya Uhuru, ambapo haki za Wafanyakazi, Wafanyabiashara, Wakulima na Wafugaji, zimekuwa zikiporwa, wajipange tuvuke Ng’ambo ya Mto.

Aidha aliwataka Wananchi, Viongozi wa Dini, akina Baba, Wazee, akina Mama na Vijana wa Jimbo la Mvomero, wasiichezee nafasi hii ambayo Mungu amewapa Wana Mvomero, wakabaki kuzunguka kwenye Mlima wa Seiri, ila wageuke upande wa Kulia uliko Ukombozi wa Mungu.

‘Wana Mvomero, Mlivyozunguka Mlima huu (wa adha na dhuluma za CCM kwa Miaka 50 ya Uhuru) Vyatosha, geukeni pande wa Kaskazini.”alisema Mchungaji Mlay, akinukuu Maandiko Matakatifu ya Biblia, Kumbukumbu la Torati Sura ya Pili 2 Mstari wa Tatu(Kumb.2:3).

No comments:

Post a Comment