Wednesday, August 12, 2015

Matokeo ya Chadema Ruaha-Kilombero, hadharani.

Na Bryceson Mathias, Ruaha-Kilosa.
BAADA ya kuwepo Mizengwe na Mamluki toka nje ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kata ya Ruaha Kilombero kutaka kuvuruga Uchaguzi wa Mgombea wa Udiwani, hatimae Mshindi wa Matokeo ya Mnyukano wa Uchaguzi huo, sasa yamewekwa Hadharani.

Akizungumza na Tanzania Daima, Katibu wa Chadema Kata ya Ruaha, Joramu Zacharia , almtaja , Isaack Maliwa, kuwa ndiye Mshindi kwa kujikusanyia Kura (43), akiwashinda, George Banda (40), Ally Mponda (6), Mathias Luambano (4), Kilango Mshana (0) na Manji Mbando (0).

Uchaguzi huo uliwahusisha Wagombea Sita (6), ambapo wapiga kura walikuwa 95, wakiwa ni Wajumbe toka katika Vijiji Vinne (4) vya, Ruaha, Simbalembende, Nyanvisi na Kising’a, vikiwakilishwa na Wenyeviti wa Vitongoji na wajumbe wa Baraza la Kata ya Ruaha.

Akiwashukuru Wajumbe Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kilosa, Kamanda Libenaga, alisema Kata ya Ruaha ndiyo yenye Chachu ya Mabadiliko, ambayo kwa sehemu kubwa itasaidia kupata Ushindi wa Ubunge wa Jimbo la Mikuni kwa sababu ina watu wengi.

Mshindi wa Uchaguzi huo, Maliwa, aliwashukuru Wapiga Kura wote, huku akikiri kuwa ulikuwa na ushindani Mkubwa, ambapo alisema kama Chama kitaridhia na kumpitisha apeperushe Bendera ya Chadema katika Uchaguzi huo, atashirikiana na Wagombea wote kuhakikisha Wanapata Ushindi wa Kata ya Ruah na Jimbo la Mikumi.

Hata hivyo, Maliwa aliahidi, “Kama Chadema kitampisha Kugombea Uchaguzi wa Kata ya Ruaha, Mshindani wake aliyemfuatia, Banda, atakuwa Kampeni Meneja wake, ili kwa Umoja na Mshikamano wao, ulete Mabadiliko Makubwa zaidi”.alisema Maliwa.

Kauli hiyo iliungwa Mkono na Mshindani wake Banda, ambaye bila Kinyongo huku wakikumbatiana, alikubali kushirikiana na Mshindi huyo, endapo atapitishwa na Chama chao, ambapo Wajumbe na Wasimamizi wa Uchaguzi huo, walipendezwa na Mshikamano na Umoja ulioonyeshwa.

No comments:

Post a Comment