Friday, July 24, 2015

TASWIRA: MAPOKEZI YA ESTHER BULAYA NA JAMES LEMBELI BUNDA.

Msafara wa bodaboda uliowapokea Mh Esther Bulaya na Mh James Lembeli walipofika Bunda kwa ajili ya kuhutubia mkutano mkubwa Jimboni Bunda.


Mh Esther Bulaya akisalimiana na Viongozi wa Chadema Bunda waliokuja kuwapokea.

Mbunge wa Viti Maalumu wa CCM aliyehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ester Bulaya akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya zamani Mjini Bunda mkoani Mara.

Mbunge wa Kahama mkoani Shinyanga, James Lembeli aliyehama kutoka CCM na kujiunga Chadema, akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya zamani ya mabasi Mjini Bunda jana

Umati wa wananchi wa Mji wa Bunda na viunga vyake, wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Stendi ya zamani ya mabasi mjini Bunda jana, uliohutubiwa pia na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya na mwenzake wa Kahama, James Lembeli waliotoka CCM na kuhamia Chadema.

No comments:

Post a Comment