Friday, April 20, 2012

DIWANI MWINGINE SENGEREMA AHAMIA CHADEMA

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Lugata (CCM) Wilaya ya Sengerema Adrian Tizeba amekihama chama hicho na kuhamia CHADEMA,

Diwani huyo kwa sasa yuko na Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godbless Lema pamoja na Katibu wa Chadema Kinondoni wakielekea kwenye mkutano wa hadhara Mjini Geita ambapo atakabidhiwa kadi yake mpya ya CHADEMA na Katibu wa Mkuu wa chama hicho Mh. Wilbrod Slaa,


Kwa Mujibu wa Mh. Lema, kesho atawatangaza Madiwani wengine wanne wa Jimbo la Sengerema (CCM) wakiwa na wenyeviti 22 wa vitongoji pamoja na wanachama wao ambao kwa pamoja wamehamua kukihama Chama cha Mapinduzi na Kuhamia CHADEMA wakilalamika kufilisikia kimawazo na kimtazamo kwa kilichokuwa Chama chao.



Pichani Diwani Tabasamu, aliyevaa kombati, akikumbatiwa na makamanda


CHANZO - Arusha Mambo

No comments:

Post a Comment