Monday, September 24, 2018

Taarifa kwa umma kuhusu hafla ya uzinduzi wa Sera za Chama toleo la Mwaka 2018.

  Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA.   

Taarifa kwa umma kuhusu hafla ya uzinduzi wa Sera za Chama toleo la Mwaka 2018.   

Tarehe 25.09.2018 Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe ataongoza tukio la kuzindua Sera za Chama toleo la Mwaka 2018.

Katika kufanikisha tukio hilo wadau mbalimbali wamealikwa zikiwemosekta na taasisi mbalimbali za umma, sekta binafsi, taasisi na asasi za kimataifa, Balozi mbalimbali, Vyombo vya Habari, taasisi za dini na taasisi za kitaaluma.     

Aidha tumealika Vyombo na taasisi mbalimbali za Serikali kama Mkuu wa Jeshi la Polisi, Gavana wa Benki Kuu, Msajili wa Vyama vya siasa na taasisi nyingine kadhaa za ndani.    

Katika uzinduzi huo ambapo Chadema itaweka hadharani misimamo ya kisera kwenye maeneo mbalimbali ya uchumi, afya, elimu na sayansi, miundombinu, maji, mfumo wa Utawala, Katiba na haki za binadamu, Masuala ya Muungano,  Mambo ya Nje na Uhamiaji, Siasa za ndani, Usimamizi wa Ardhi  na Kilimo pamoja na Mazingira.                         

Aidha baada ya mialiko mbalimbali kuwasilishwa kwa wadau mbalimbali, tumestushwa na taasisi ya Elimu  (Chuo Kikuu cha IFM) kutoa tangazo na kulilipia kwenye Vyombo vya Habari kuwa wao sio taasisi ya kisiasa na hivyo hawatashiriki kwenye uzinduzi huo.                        

Kama Chadema tunaamini kuwa taasisi zetu za elimu zina wajibu wa kusoma na kufanya tafiti mbalimbali za kisomi kuhusu Sera za Vyama vya siasa ili waweze kuwajibu kwa ufasaha wanafunzi wao kuhusu Sera za Vyama na utekelezaji wake, hivyo hawapaswi kujitenga na michakato ya kisera ya Vyama vya Siasa kwani Sera huzaa dira na mipango ya Maendeleo ya Taifa.     

Tunawaalika wadau wote wa Maendeleo ya taifa wazipitie Sera zetu na kutoa maoni, ushauri na mapendekezo kwani tunajenga Taifa moja.                     


Imetolewa na;

John Mrema - Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

24 Septemba, 2018

No comments:

Post a Comment