Wednesday, August 22, 2018

Kuujua uwezo wa Sir Alex Ferguson, inaweza kukusaidia kumjua kocha wa siasa za Tanzania Sir Freeman Aikael Mbowe.



Na
Mwalimu John Pambalu.

Dunia imeshuhudia uwezo wa ajabu wa viongozi wawili , mmoja akiwa kocha wa timu ya wa club ya Manchester united ya nchini uingereza na mwingine akiwa kocha wa siasa za taifa la Tanzania Sir Freeman  A. Mbowe.

Ferguson meneja wa zamani wa club ya Manchester united alipata heshima kubwa kwa kuvunja rekodi ya kuinoa timu ya Manchester united kwa miaka takriba 27 kwa mafanikio makubwa.

Mbowe pia ndiye mwanasiasa bora zaidi nchini Tanzania na Afrika ya mashariki kwa kukiongoza chama kikuu cha upinzani kutoka mwaka 2004 mpaka sasa kwa mafanikio makubwa sana. Ameitoa chadema kutoka chama kisichokuwa na uwezo wa kusimamisha mgombea urais (chama cha  kudandia wagombea wa NCCR MAGEUZI mwaka 1995 na chama cha CUF mwaka 2000) mpaka kufikia hatua ya kusimamisha wagombea urais mwaka 2005,2010 na 2015 huku matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 yaliyotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi yakidai eti Chadema ya Freeman Mbowe ilipata zaidi ya kura 6,000,000 tu dhidi ya 8,000,000 za CCM.

Ferguson anakumbukwa zaidi na washabiki wa soka duniani kote kwa mataji aliyobea kama mataji 13 ya ligi ya uingereza, 2 ya klabu bingwa ulaya na 5 kombe la FA. Aidha Ferguson anakumbukwa zaidi kwa uwezo wake wa kuibua kulea na kuendeleza vijana chipukizi kama wakina  *David Beckham, Christian Ronaldo, Van der sar, Ferdinand, Vidic, Evra, Rooney, Giggs* na wengine wengi.

Pia Freeman Mbowe anaheshimika zaidi kwa kuibua, kulea na kuendeleza vijana kama  *John Mnyika, John Heche, John Mrema, Benson Kigaila, Halima Mdee, Ezekia Wenje, Zitto Kabwe, David Silinde* na wengine wengi.

Siraha kubwa wanayoitumia miamba hii ya mifumo ya ushindi ( Ferguson na Mbowe ) ni kusimamia nidhamu kuliko tukuka.

Mwaka 2009 Christian Ronaldo akiwa mchezaji bora kuliko wote duniani alitaka kujiona yeye ni bora kuliko timu. Ferguson akaamua kumuuza ili kuwafundisha wachezaji wanaobaki kuwa hakuna supper star zaidi ya timu ya Manchester united. Maamuzia kama haya yalifanywa mwaka 2015 dhidi ya Dr. Slaa aliyekuwa katibu mkuu mahiri sana. Mbowe akasimamia maamuzi ya vikao kwamba hayupo aliye bora zaidi ya Chadema.

Aidha vuguvugu la wanaaiasa wa upinzani kuhama vyama vyao masalani Chadema na kujiunga na CCM, pia yanathibitisha uwezo wa Freeman  Mbowe.

Itakumbukwa kuwa utaratibu wa kupitisha wagombea wanaowania nafasi za uwakilishi bungeni na katika halmashauri, wawakilishi wa vyama hupitishwa baada ya kupigiwa kura za maoni ndani ya vyama.

Umefika wakati wawakilishi wakijiudhuru kutoka Chadema wanateuliwa na CCM bila kupitia mchakato wa kura za maoni.

*Hii ni ishara wazi kuwa hata CCM wanatambua kuwa vijana waliopita mikononi mwa Mbowe wanauwezo mkubwa kuliko vijana na wazee walioko CCM.*

Ndio maana wanaotokea  Chadema wanapata teuzi za ukuu wa wilaya, ukatibu tawala nk. Huku waliokulia CCM  wakiendelea kuzeeka bila teuzi.

Ferguson na Mbowe wanabaki kuwa alama ya uwezo wa taasisi walizoziongoza (Manchester United na Chadema)


Tangu alipong'atuka madarakani Ferguson mpaka leo club ya Manchester united imepoteza mwelekeo wake, kosa ambalo taasisi ya Chadema haiko tayari kulifanya hata kidogo.

Wasalaam 
John Pambalu.
Diwani wa kata ya Butimba Mwanza
Makamu Mkt Bavicha Tanzania bara.
Mshabiki wa Manchester United



No comments:

Post a Comment