Wednesday, October 25, 2017

UJUMBE KUTOKA KWA TUNDU LISSU

Mambo haya ni mazito na Msikimbilie kuwa na hasira, kwani hasira hasara


1. Kwanza ningependa niwasalimie wapenzi na wanachama wa UKAWA kwa ujumla wenu nashukuru kwa meseji zenu ambazo nimezipata ni 297,576 (laki mbili tisini na saba elfu na mia tano sabini na sita). Ingawa nimejitahidi kusoma nyingi, na Bado napitia zingine.

2. Na wengi wao wana lalamika mbona UKAWA (Chadema) hamchukui hatua kwa udhalimu na Visasi mnaotendewa?

3. Ila niwajibu hivi :-
Mnakumbuka Raisi wa zamani Laurent Gbagbo wa Ivory Coast alivyoshindwa uchaguzi ili alilazimisha tume yao ya uchaguzi wamtangaze ameshinda uchaguzi ule, Na tume ile kwa sababu ilikuwa sio huru, iliteuliwa na na yeye, na waliogopa kutenguliwa kipindi kile walimtangaza kuwa yeye Laurent Gbagbo ni mshindi badala ya mshindi halali ambaye alikuwa Alassane Ouattara na sasa ameshitakiwa Mahakama ya ICC, Kwa hiyo haya ni mambo ya muda tu.

4. Mfano wa pili ni Samweli Doe wa Liberia ambaye baadaye alipinduliwa na rafiki yake ambaye alikuwa na jeshi dogo lakini wananchi walimuunga mkono kutokana na kupinga udhalimu uliokuwa ukitendwa na watu wake Samweli Doe.

5. Ila sisi Upinzani hatupendi tuingie kwenye Vurugu za kuhatarisha Amani ya nchi ingawa tuna bambikizwa na kesi za uchochezi kila kukicha na tunasikia tu kuwa wao wanapokea amri kutoka Juu kwa hiyo wanatimiza amri hiyo.

6. Ila niwaambie neno moja tu kutokana na utafiti huu Dikteta anajimaliza mwenyewe, huku wapiga vigelegele wake wakimpoteza.

7. Napenda mfahamu pia kuwa sio watu wote waliopo kwenye system hiyo ya kidikteta wanafurahia matendo hayo yote tunayofanyiwa , na wanatupatia taarifa ya mambo wanayotaka kutufanyia.

8. Mambo haya ni mazito na Msikimbile kuwa na hasira, kwani hasira hasara.

9. Madikteta wengi huwa wana chuki na visasi moyoni mwao na vitu wanavyofanya huwa wanafanya kwa malengo yao maalum na kupanga safu yao uongozi kwa malengo maalumu mfano:-

10. Wanaweza kuweka kikwazo Fulani fulani au kuleta kitu fulani ili vurugu ifanyike ili wao wapate sababu au kisingizio cha kumpata mtu Fulani ili kulinda maslahi yao, kama vile kumkamata mtu na kumtia kizuizini ili lengo Fulani litimie kama ushindi wa uchaguzi, au vinginevyo, na pia kuvipunguzia nguvu vyama fulani au kuviua nadhani mmeona kwa kupitia kwa Bwana Yule.

11. Inafahamika wazi kabisa kwao kuwa watu wameshajua mambo yao mengi na Madikteta wanajua kuwa hawakuingia madarakani kwa ushindi halali, hali inayowapa presha na kufanya mambo kwa kukurupuka ili kuokoa jahazi, pia kukwamisha maendeleo kwenye Miradi au mipango kwenye maeneo ya wapinzani.

12. Napenda niwasihi makamanda wote na wapenzi wa UKAWA tuwe na Busara kwani Afrika tuko kwenye hali mbaya sana,na Tufahamu kuwe Dikteta anjimaliza mwenyewe, ni swala la Muda tu.

13. Kuna Vilio kila kona na kila idara, na kwa mujibu wa utafiti Dikteta atajimaliza mwenyewe kama wengine walivyojimaliza. Historia huwa inajirudia.

No comments:

Post a Comment