Wednesday, August 23, 2017

HALI YA ESTER BULAYA INAENDELEA VIZURI BAADA YA KUPATIWA MATIBABU

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Mh. Edward Lowassa amefika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dar kumjulia hali Mbunge Ester Amos Bulaya.


Dar es Salaam
. Hali ya Mbunge wa Bunda Ester Bulaya aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH ) inaendelea vizuri baada ya kuanza kupatiwa matibabu jana.

Bulaya ambaye alipata tatizo la kupumua baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu ya Kituo cha Kati cha Polisi mjini Tarime, alifikishwa hospitalini hapo juzi usiku na kulazwa katika wodi namba 18 Sewahaji.

Akizungumza Ofisa Uhusiano wa Muhimbili, John Stephen alisema leo Bulaya amepata ahueni kiafya na anaendelea vizuri na matibabu.

"Sasa ameanza kujihudumia mwenyewe, anakula vizuri na bado anaendelea na matibabu," amesema Stephen huku akisisitiza kuwa mgonjwa bado anahitaji utulivu kwa kipindi hiki.

Bulaya amesota rumande tangu akamatwe Ijumaa ya Agosti 18 kwa madai ya kuingia jimbo la Tarime na kufanya shughuli za kisiasa kwa kutoa msaada wa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika shule za msingi jimboni humo baada ya kualikwa na mbunge mwenzake Ester Matiko

Mwananchi

No comments:

Post a Comment