Wednesday, May 3, 2017

UTEUZI WA WAGOMBEA UBUNGE EALA

TAARIFA KWA UMMA



UTEUZI WA WAGOMBEA UBUNGE EALA

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyokutana Zanzibar katika kikao chake cha siku moja, Mei 2, mwaka huu, imewateua wafuatao kuwa wawakilishi wa CHADEMA kugombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA);

1. Profesa Abdalla Safari
2. Salum Mwalim
3. Ezekia Wenje
4. Josephine Lemoyan
5. Lawrence Masha
6. Pamela Massay


Walioteuliwa watakamilisha hatua zingine za uteuzi kwa mujibu wa taratibu na Kanuni za Bunge na Uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki.


Imetolewa leo Jumatano Mei 3, 2017 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

No comments:

Post a Comment