Wednesday, February 22, 2017

MAHAKAMA KUU YAZUIA MBOWE ASIKAMATWE

Februari 21, 2017 Mahakama Kuu imeamuru Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe asikamatwe hadi maombi yake kutokamatwa yataposikilizwa siku ya Ijumaa.

Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni tarehe 10 mwezi huu alifungua kesi ya Kikatiba dhidi ya RC Paul Makonda, Kamanda Simon Sirro.

Aidha Mahakama imewaushauri upande wa mlalamikaji kurekebisha hati ya mashtaka kisha wairudishe tena siku ya Jumatatu.

Siku ya jana Mawakili wa Mbowe waliweka pingamizi la kutokamatwa kwa kiongozi huyo lakini kabla taarifa hazijalifikia Jeshi la Polisi, Mbunge huyo wa Hai akatiwa nguvuni

No comments:

Post a Comment