Thursday, May 5, 2016

Naibu Spika amemtoa nje Mbunge wa Ukonga (CHADEMA), Mwita Waitara

Naibu Spika wa Bunge La Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson leo amewaamuru askari wa Bunge kumtoa Bungeni Mbunge wa Ukonga Mwita Waitara baada ya mbunge huyo kutaka kumfanyia fujo mbunge wa Kasulu Vijijini Augustine Vuma Holle wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria

Leo Dodoma, Wizara ya Katiba na Sheria ilikuwa ikiwasilisha mpango wa makadirio ya bajeti kwa mwaka 2016/2017 kupitia kwa Waziri wake Harrison Mwakyembe.

Baada ya kuwasilisha kazi ikawa ni zamu ya Wabunge kuchangia bajeti hiyo, lakini hali ikabadilika wakati Mbunge wa Kasulu Vijijini Augustino Hole alivyopata nafasi ya kuchangia akaanza kwa kutoa kauli kuwa ‘Tundu Lissu ana cheti za Milembe‘ kauli ambayo ilionyesha kutowapendeza baadhi ya Wabunge wa kambi ya upinzani.

Ghafla Mbunge wa Ukonga Mwita Waitara akainuka na kuanza kupiga kelele kuonyesha kutofurahishwa na kauli hiyo kisha kuanza kusimama na kuanza kupiga meza. Naibu Spika Tulia Ackson Mwansasu akamtaka mbunge huyo kukaa chini, Waitara hakuonyesha kutii amri ndipo Naibu Spika akaamulu askari Polisi wa bunge kumtoa nje ya bunge.

No comments:

Post a Comment