Tuesday, January 19, 2016

MEYA WA MANISPAA YA KINONDONI AANZA KAZI RASMI

Meya mpya wa Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Boniface Jacob, ameanza majukumu yake mapema leo 18 Januari ya Umeya huku akikumbana na umati wa wananchi waliofika kumuona kwa malalamiko ya migogoro ya ardhi ambayo ni changamoto katika Manispaa hiyo.

Hata hivyo Meya huyo baada ya kuwasili ofisini kwake na kupokelewa na baadhi ya maafisa kadhaa wa Manispaa hiyo na kutinga kwa mara ya kwanza ndani ya ofisi ya Meya ambayo atakuwa akiitumia kwa kipindi chote, baada ya saa chache kundi la wananchi kutoka Wazo Block B, walifika katika ofisi hiyo kwa lengo la kumuona ilikumweleza kero zao ambazo wamedai kuwa wafanyakazi na watendaji wa Manispaa hiyo wamepora maeneo yao na kuwauzia wafanyabiashara wengine.


Kwa busara ya Meya Boniface Jacob, ameweza kusikilza kero za wananchi hao huku akiahidi kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu hadi hapo haki itakapopatikana. Ambapo amewaomba wananachi hao wasubirie kuona kama Manispaa ilifanya tathimini na nani aliuza viwanja hivyo na fedha ziliingia wapi ambapo ametoa agizo kwa Mtathimini na afisa ardhi wa Manispaa kuanza mara moja kukagua kujua nani ameusika kwenye mgogoro.

Wakazi hao zaidi ya 50, wanaeleza kuwa, mgogoro huo umeendelea kudumu zaidi ya miaka 15 sasa huku mara zote wamekuwa wakizungushwa pasipo kupata haki zao. Pia wameeleza kuwa, miongoni mwa wananchi wanaokaa kwenye maeneo hayo wamekuwa wakiishi kwa hofu ya kuvunjiwa nyumba zao kwani baadhi ya watu wamekuwa wakifika na kuwapa taarifa kuwa maeneo hayo ni ya mwekezaji huku wengine wakitumia ubavu kuvunja nyumba za wananchi pasipokuonyesha hati halisi kitendo ambacho wamekiona kuwa Watendaji wa Manispaa hiyo kuuza kinyemela viwanja vyao.

Pia wananchi hao wamewataia baadhi ya vigogo wa Serikali wakiwemo watendaji wa Manispaa hiyo ya Kinondoni kwa kujimilikisha maeneo ikiwemo kujenga nyumba katika ardhi ya wananchi hao.




No comments:

Post a Comment