Thursday, December 10, 2015

Muasisi wa Chadema ampa tano Rais Magufuli

WATANZANIA wa Kada mbalimbali wamempongeza Rais John Magufuli kwa kuokoa mamilioni ya shilingi ambayo yangetumika kwenye maazimisho ya miaka 54 ya uhuru wa Tanzania, Anaandika Faki Sosi…(endelea).

Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia Muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, amesema kuwa uamuzi wa Rais Magufuli wa kufuta sherehe za uhuru utakuwa umeleta tija kubwa kwa taifa ambapo miaka mingi taifa limekuwa likichezea mabilioni ya shilingi bila faida kwa taifa.

Mtei alimesema kuwa sherehe hizo zilizokuwa zikifanyika kwa shamrashara ambazo zilikuwa zinagharimu fedha za walipa kodi kwa anasa za kula,kunywa na kulewa huku watanzania wakikosa huduma muhimu.

Aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF),Profesa Ibrahim Lipumba ameshauri kuwa sherehe hizo zifanyeke mara moja kila baada ya miaka mitano ambapo zisihusishe matumizi mabaya ya fedha za wananchi kama zilivyokuwa za awamu iliyopita kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii.

Naye spika wa kwanza wa Bunge la Tanzania Pius Msekwa amesema kuwa kitendo hicho kinapaswa kuungwa mkono kwa kila ambaye anayeitakia mema Tanzania. Sherehe hizo zimewaunganisha waatanzania wote kwa kufanya jambo moja ambapo sherehe hizo zilikuwa zikifanyika Dar es Salaam pekee kwa gharama kubwa lakini sasa zimekuwa za nchi nzima na zenye maslahi na taifa.

MwanaHalisiOnline

No comments:

Post a Comment