Saturday, July 19, 2014

KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA

Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana jijini Dar es Salaam kwa siku mbili kuanzia Ijumaa ya tarehe 18-19 Julai, 2014, katika kikao chake cha kawaida kwa mujibu wa Katiba ya Chama.

Katika siku mbili hizo, wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA watajadili pamoja na masuala mengine;

· Mchakato wa Katiba Mpya.

· Taarifa ya hali ya siasa nchini.

· Uchaguzi wa ndani ya chama.

· Taarifa ya fedha, Mpango Kazi na Bajeti.

· Mapendekezo ya marekebisho ya Katiba, Kanuni na Miongozo ya Mabaraza ya Chama.

· Maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

· Taarifa ya Katibu wa Wabunge.

· Rufaa mbalimbali.

· Nembo na Kadi za Mabaraza ya Chama.

Kikao hicho kitatanguliwa na hotuba ya ufunguzi ambapo vyombo vya habari vinaalikwa kuhudhuria.

Imetolewa leo Alhamis, tarehe 17 Julai, 2014 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari- CHADEMA




No comments:

Post a Comment