Thursday, May 30, 2013

Waziri Kabaka; Wawekezaji wanajifanya wako juu ya Watanzania.

INGAWA Waziri wa Kazi na Ajira Gaudensia Kabaka (MB) kasema mifuko ya hifadhi iko kwenye hali nzuri na ni endelevu, Ingawa kuikweliiko kwenye hali mbaya, mfuko wa Pensheni ya wafanyakazi (PPF) ni Janga kwa wastafu na wafanyakazi wa Mashambani na Kilimo.
Siafikiani na Waziri Kabaka kwamba Migogoro sehemu za kazi imepungua kwa kutumia maridhiano ya chombo cha kutatua Migogoro(CMA), bali ndiyo kwanza imeongeza na tena ni mibaya kuliko ile ya awali kwa sababu Wawekezaji wanajifanya wako juu ya watanzania.
Katika michango ya Wabunge kwenye Bajeti ya Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira, waliitaka Serikali na Wizara Ichukue hatua Kali dhidi ya Mifuko inayochelewesha Michango ya Wafanyakazi, Jambo ambalo Waziri Kabaka alikiri kuwapo kwa tatizo hilo.
Nimsadie Waziri Kabaka, Waajiri na hasa Wawekezaji ambao hivi sasa wanajifanya kuwa wako Juu ya Wafanyakazi na Watanzania, wamekuwa na nguvu ya kuwadhulumu na kukaa na Michango ya Wafanyakazi au Mafao ya Wastaafu, kwa sababu ya Kiburi ya Fedha.
Kiburi ya Fedha, imesababisha baadhi ya Watoa maamuzi tangu Ngazi za Wizara ya Kazi kuwa kama Vipofu wasioona udhalimu na Viziwi wasiosikia, Malalamiko ya aina yoyote inayotolewa na wafanyakazi na Wastaafu, jambo lililopiga hodi hadi Serikali Kuu.
Mfano; Mwekezaji wa Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa kupitia Mfuko wa PPF, kwa miaka kadhaa amekuwa hapeleki michango ya wafanyakazi wake tangu alipobinafshiwa Kiwanda, asilimia 5% waliyokatwa wafanyakazi kwenye mishahara, na 15% anayotakiwa atoe mwajiri.
Kimsingi wafanyakazi zaidi ya 100 wa mtibwa, wameshafariki bila kupata mafao yao, ambapo hata wajane au wagane waliobakia, wameendelea kunyanyasika wasiyapate mafao hayo hadi leo, na waliopata kiasi, wamepewa kwa mafungu kama Nyanya za sokoni, fedha zikitumika.
Inatafsirika kuwa, baadhi ya vigogo na wastaafu serikalini wenye sauti na hisa ya uwekezaji huo, cha kusikitisha wamehusishwa katika dhuluma na manyanyaso ya haki za wafanyakazi na wastaafu hao, ambapo kwa dhuluma hizo huko mbinguni tutakuwa Kuni.
Kama kuna mfuko ambao siupendi moyoni mwangu na hata kuuona, basi ni PPF. PPF wameshiriki kudhulumu haki za wafanyakazi wa mtibwa. Kwa muda mrefu nadhani ni kuwaheshimu baadhi ya vigogo wastaafu, kiasi wamepora michango ya wafanyakazi na wastaafu.
Wengi wao wamekufa kwa kihoro na mwingine aliyekuwa alipwe Mil. 13/- kufanya kazi miaka 14; alipwe Mil. 2.5/-, jambo lililowafanya vijana wengi wenye nguvu kuacha kazi na kufanya kazi za kujiajiri au kwenda kwingineko; mmoja wao  ni Mkurugenzi wa kufuatilia Mwenendo wa Bunge Marcossy Mgweno.
Sisemi kama wanavyoambiwa viongozi na wananchi nchini wasioijua mtibwa ilivyo. Ninao ushahidi na ninaweza kuutetea. Utetezi wa awali Mtibwa 2005 ilihukumiwa na Mahakama ya kazi kumlipa kila mfanyakazi aliyedai Sh. 500,000/- kwa kuchewesha Michango.
Ieleweke, Mgeni aliyelala Kiangazi nyumba inayovuja, hawezi kujua kuvujiwa na adha ya Mvua katika nyumba hiyo; Akiamka kuendelea na safari, ataishia kuisifu kwa kumtunza usiku ule, lakini ingekuwa wakati wa Mvua angeilaani.
Aidha Waziri Kabaka Mwenyewe, akiwa Naibu Waziri, alishindwa kutatua migogoro na maatatizo ya wafanyakazi na wastaafu wa Mtibwa mara mbili, ambapo alijua dhuluma na unyanyasaji unaoendelea kufanyika, huku viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakila asali.

No comments:

Post a Comment