Thursday, May 30, 2013

Shehe apasua jipu la udini mkutano wa CHADEMA Uwanja wa Zakhem Mbagala

Aliwataka wananchi wa Kata ya Mianzini, Mbagala, Temeke Dar es Salaam kutofanya makosa kusikiliza propaganda za udini za CCM na kile chama kingine walichoungana nacho, Shehe Juma Mwipopo ametoa kauli nzito hapa akisema Serikali ya CCM ndiyo imeleta chokochoko zinazoendelea nchini.

Amesema kuwa siku zote viongozi wa CHADEMA wamesimamia na kuzungumzia maisha ya watu, si ukristo wala uislamu wao.

Amesema kule bungeni, Makamanda wa CHADEMA, chini ya uongozi wa Mwenyekiti na KUB Mbowe, akina Mnyika au Zitto hawazungumzii ukristo wala uislamu wao, bali maisha ya Watanzania, maisha ya binadamu, maendeleo ya watu.

Amesema kama ni udhalilishaji wa dini, na hasa viongozi wa kiislamu, CCM na serikali yake ndiyo wanaongoza

"Waislamu wenzangu ninyi ni mashahidi, alipokufa Michael Jackson, Rais Kikwete alimpigia simu Spika wa Bunge, Sitta asimamishe bunge ili kuomboleza, lakini bunge hilo hilo halikuomboleza kifo cha Naibu Mufti, Shehe Gorogosi...mnakumbuka namna ambavyo serikali hii ya CCM ilimzika Steven Kanumba, lakini hawakuweza hata kuhudhuria kwenye msiba wa Shehe Gorogosi ambaye alikuwa naibu mufti wetu...juzi juzi hapa mmeona msanii Lulu alituhumiwa kesi nzito ya mauaji, baadae kapata dhamana, lakini Shehe Ponda kanyimwa dhamana.

"Mnajua Watanzania wenzangu, Shehe Ponda alipokamatwa na kunyimwa dhama visivyo na serikali ya CCM watu wa kwanza kuzungumzia uminywaji huo wa haki walikuwa ni CHADEMA, wajumbe wa Kamati Kuu, Mabere Marando na Profesa Abdalla Safari, wakasema hiyo ni kinyume cha haki na sheria za nchi. Majuzi pia mmesikia Zitto kazungumza bungeni, akionesha namna ambavyo Waislamu wamenyanyaswa, ikiwemo tukio la Mwembechai, Zitto kazungumza Jumatano, Alhamis,onda kaachiwa mahakamani.

"Hivi ndivyo CHADEMA wanafanya kazi, chini ya uongozi wa Katibu Mkuu wetu hapa, Dkt. slaa, wanazungumzia haki na ukweli kwenye maisha ya watu, maisha ya Watanzania. Wamepinga ufisadi. Mambo haya yote uamezungumziwa katika vitabu vyote vya dini, kupigania haki, kupigania ukweli, kupinga dhuluma, ufisadi na wizi. Hii ndiyo kazi ya CHADEMA chini ya viongozi wetu makini. Msikubali kudanganywa na CCM na serikali yake na CUF. " alisema Shehe Mwipopo ambaye ni Katibu wa CHADEMA, Wilaya ya Ukonga.




No comments:

Post a Comment