Wednesday, May 29, 2013

Sekondari ya Mpwayungu yafungwa kwa ukosefu wa Maji.

Walimu na Wanafunzi wa Sekondari ya Mpyayungu Kata hiyo Manispaa ya Dodoma, wanajiandaa kurudi makwao baada kulazimishwa kuwahi kufunga kutokana na ukosefu wa maji.
Malalamiko hayo yametolewa jana 28.5.13 na Walimu na Wanafunzi wa shule hiyo, kutokana na baadhi yao kuanza kuumwa matumbo na kuhara kutokana na kutumia maji machafu wanayochota visimani.
Wakizungumza kwa masikitiko ya kuwahi kufunga wakati bado wana wana majaribio ya mitihani Wanafunzi na Walimu hao walimlaumu Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, Gabriel Hoya, kwa kushindwa kutengeneza Mashine ya kusukuma maji kwa sababu zisizoeleweka.
“Hii ni mara ya nne sasa walimu na wanafunzi wanapata adha za namna hii, ambapo hata viongozi wa Kata wanaonekana kutotilia maanani usumbufu unaowakabili walimu na wanafunzi katika masomo”. Alisema mmoja wa walimu aliyeomba asitajwe.
Mwandishi alimtafuta mwalimu mkuu wa Sekondari, Andew Honya, aliyekiri kuwepo kwa tatizo na kusema wanalazimika kufunga shule mapema kutokana na ukweli huo ambapo alisema wanaogopa magonjwa ya kuambukiza yasitokee shuleni hapo
Hata afisa elimu wa Shule za Sekondari wilaya ya Chamwino. Valentine Christopher, nimemuarifu na ameruhusu hatua hiyo na kuridhia ifanyike ili kuweka Kinga badala ya kukaribisha madhara.
Afisa Elimu Sekondari Christopher, alipotafutwa ajibu mkasa huo simu yake ilikuwa haipatikani, na  msaidizi wake, Hamisi Mapoto, pia hakupatikana, ambapo Afisa Elimu Msingi,  Scolar Kapinga, simu yake iliita lakini hatukuweza kusilizana kutokana na mwandishi kuwa juu ya mti ili apate mawasiliano.

BRYCESON NYEREGETE

No comments:

Post a Comment